Saturday, March 17, 2012

Dalili 4 za mwanaume aliye tayari kwa maisha ya ndoa

Ukijaribu kuchunguza utabaini kuwa wanaume wanaoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na kuoa kila siku ni wengi lakini je wanaoolewa wote wanaingia kwenye maisha ya ndoa na watu sahihi? Jibu ni hapana, na hii ni kwa sababu wanawake wengine wanakubali kuolewa na wanaume ambao hawakujiandaa kuingia kwenye maisha hayo. Dalili zenyewe ni hizi hapa chini.


Waliobaini kuwa ni muda mufaka
Unaweza kuwa kwenye uhusiano na mwanaume ambaye umri wake umekwenda lakini bado anaona anastahili kuwa kwenye maisha ya ‘ubachela’. Ukikubali kuolewa na mwanaume wa sampuli hii lazima atakusumbua lakini yule ambaye amekaa, akatafakari kisha akagundua kuwa ni wakati muafaka wa kuoa, ni wazi huyo atakuwa amejiandaa na hata ukimkubalia sidhani kama utajuta.

Anajiamini, siyo tegemezi
Ni kweli mapenzi hayana uhusiano wowote na fedha lakini ukweli usiofichika ni kwamba kama mwanaume hana kazi inayomuwezesha kumuingizia kipato, hawezi kuwa miongoni mwa wale wanaostahili kuingia kwenye maisha ya ndoa.
Ukikubali kuolewa na mwanaume asiye na kitu eti kwa sababu tu umempenda na moyo wako hauko tayari kumkosa, ujue unajiingiza kwenye maisha ya bahati nasibu kitu ambacho siyo kizuri. Kama huyo uliyenaye siyo tegemezi, ni mtu mwenye uwezo wa kukulisha na kukutimizia shida zako zinazohitaji fedha, usione hatari kumwambia afanye hima akatoe mahari muoane.

Anachukua nafasi ya baba
Kuna baadhi ya wanaume licha kwamba hawajaingia kwenye maisha ya ndoa na hawajafanikiwa kuwa na watoto lakini wameshaanza kuzishika nafasi za ‘ubaba’. Unaweza kuwa na mpenzi akawa ni mtu wa kupenda sana watoto na wakati mwingine kuzungumzia namna wa kwake watakavyokuwa. Huyu ni mwanaume ambaye ana dalili za kutaka kuingia kwenye maisha ya ndoa.

Anakuchukulia kama mke wake
Chukulia kwamba uko na mpenzi wako lakini jinsi anavyokuchukulia ni kama mke wake. Kwa kifupi utaanza kumuona anachukua nafasi ya mume. Kwa mfano ataanza kuweka mikakati kwa ajili ya maisha yenu ya baadae, atakutambulisha kwa ndugu, jamaa na marafiki zake, atakuwa akikushirikisha katika kila suala linalogusa maisha yako na yake.
Aidha, mtaalam wa masuala ya mapenzi nchini Marekani, Carol Morgan anaongeza kuwa, licha ya yote hayo pia mwanaume huyo atakuwa ni mkweli na muwazi katika kila jambo.
Hizo ni dalili nne za mwanaume ambaye amejiandaa kuingia katika maisha ya ndoa.

No comments:

Post a Comment