Sunday, March 18, 2012

Kusinyaa/Kuziba kwa mrija wa mkojo (Urethral stricture)

Mrija wa mkojo (urethra) ni kiungo muhimu kinachotoa mkojo nje ya mwili kutoka kwenye kibofu. Mrija huu unaposinyaa au kuziba hufanya utokaji wa mkojo kuwa wa mashaka na maumivu makubwa. Kusinyaa/ Kuziba kwa mrija wa mkojo huitwa pia urethral stricture.

Visababishi na vihatarishi vya tatizo hili
Kusinyaa kwa mrija wa mkojo husababishwa na kovu linalotokea katika sehemu ya mrija baada ya mtu kuumia, kufanyiwa upasuaji au kupona magonjwa ya zinaa. Inaweza pia kusababishwa na uvimbe karibu na eneo la kinena unaokandamiza mrija.

Vihatarishi vya tatizo hili ni pamoja na:

  • Kuwa na historia ya kuugua magonjwa ya zinaa
  • kuwahi kuwekewa mipira ya mkojo au vifaa vya namna hiyo (catheter au cystoscope)
  • Kuvimba tezi dume (BPH) kwa wanaume
  • kuwa na historia ya kuumia au kupata majeraha maeneo ya kinena. Hii hutokea sana kwa wale wanaopata ajali wakiendesha baiskeli
  • Kupata maambukizi ya mara kwa mara ya mrija wa mkojo (urethritis)

Ni nadra sana kwa tatizo hili kutokea kwa wanawake. Aidha ni nadra pia kwa mtoto kuzaliwa akiwa na tatizo hili (congenital urethral stricture).

Dalili
Mtu mwenye tatizo hili anaweza kuwa na dalili zifuatazo,

  • Kutoa shahawa zilizochanganyika na damu
  • Kukojoa mkojo mweusi au uliochanganyika na damu
  • Kupungua kwa kiasi cha mkojo kinachotolewa
  • Kukojoa kwa shida
  • kutoa uchafu katika mrija wa mkojo
  • kukojoa mara kwa mara
  • Kushindwa kumaliza mkojo wote
  • Kushindwa kuhimili kutoka kwa mkojo (mkojo kujitokea wenyewe/kujikojolea)
  • Maumivu wakati wa kukojoa
  • Maumivu chini ya tumbo
  • Maumivu ya kinena
  • Mtiririko dhaifu wa mkojo (hutokea taratibu au ghafla)
  • Mkojo kutawanyika ovyo wakati wa kukojoa
  • Kuvimba uume

Uchunguzi
Daktari atakufanyia uchunguzi wa mwili na namna unavyokojoa. Uchunguzi wa mwili unaweza kuonesha:

  • Kupungua kwa mkondo wa mkojo
  • Uchafu kutoka katika mrija wa mkojo
  • Kibofu kilichojaa/kuvimba
  • Kuvimba kwa mitoki ya maeneo ya kinena
  • Tezi dume iliyovimba au yenye maumivu
  • Kuhisi kitu kigumu chini ya uume
  • Uume kuvimba au kuwa mwekundu

Hata hivyo, wakati mwingine uchunguzi unaweza usioneshe tatizo lolote lile.

Vipimo
Vipimo ni pamoja na:

  • Kipimo cha kuchunguza mrija pamoja na kibofu cha mkojo (cystoscopy)
  • Kuangalia kiasi cha mkojo kinachobaki katika kibofu baada ya kukojo (Post-void residual (PVR) volume)
  • X-ray ya mrija wa mkojo (Retrograde urethrogram)
  • Vipimo vya magonjwa ya zinaa
  • Uchunguzi wa mkojo (Urinalysis) pamoja na kuotesha mkojo (Urine culture)

Matibabu
Mrija unaweza kutanuliwa wakati wa kipimo cha cystoscopy na hiyo ikawa ndiyo mojawapo ya tiba.
Iwapo njia ya kutanua mrija haioneshi mafanikio sana, upasuaji unaweza kuhitajika. Upasuaji unategemea eneo lilipo tatizo na ukubwa wa tatizo. Kama tatizo ni dogo/fupi na lipo mbali na bawabu inayotenganisha mrija na kibofu cha mkojo, linaweza kutatuliwa kwa kukata kasehemu kalikoziba wakati wa kufanya cystoscopy au kwa kuweka kifaa maalum cha kuzibua na kutanua mrija.

Kama tatizo ni kubwa zaidi, upasuaji wa wazi wa eneo husika unaweza kufanyika. Upasuaji huu unajumisha kukata sehemu iliyoziba na kisha kukarabati sehemu hiyo.

Kwa mgonjwa ambaye amepata shida ya ghafla ya kushindwa kutoa mkojo (acute retention of urine), matibabu ya dharura ya kumuwekea catheter kupitia juu ya kinena (suprapubic catherization) hufanyika. Hii husaidia kibofu kutoa mkojo nje kupitia kwenye bomba lililowekwa chini ya tumbo.

Ifahamike kuwa mpaka sasa hakuna dawa ya tatizo hili zaidi ya njia za upasuaji na nyingine zilizoelezwa hapo juu.

Matarajio
Mara nyingi matibabu huleta matokeo mazuri na mgonjwa anaweza kuishi maisha yake kama kawaida. Hata hivyo wakati mwingine, mgonjwa anaweza kuhitaji matibabu ya mara kwa mara ili kuondoa sehemu ya kovu iliyopo katika mrija wa mkojo.

Madhara ya tatizo hili
Tatizo hili halina budi kutibiwa haraka maana kama likiachwa linaweza kusababisha kuziba kabisa kwa njia ya mkojo na kusababisha mkojo kujaa katika kibofu, hali ambayo, pamoja na kuleta maumivu makali kwa mgonjwa inaweza pia kusababisha figo kushindwa kufanya kazi (ARF).

Kinga
Ni muhimu kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa kwa kufanya ngono salama au kuacha kabisa kufanya ngono. Aidha kuwa makini na kazi au mambo ambayo yanaweza kukusababishia kuumia maeneo ya kinena.

1 comment:

  1. Am Richard, I am here to testify about a great herbalist  man who cured my wife of breast cancer. His name is Dr Imoloa. My wife went through this pain for 3 years, i almost spent all i had, until i saw some testimonies online on how Dr. Imoloa cure them from their diseases, immediately i contacted him through. then he told me the necessary things to do before he will send  the herbal medicine. Wish he did through DHL courier service, And he instructed us on how to apply or drink the medicine for good two weeks. and to greatest surprise before the upper third week my wife was relief from all the pains, Believe me, that was how my wife was cured from breast cancer by this great man. He also have powerful herbal medicine to cure diseases like: Alzheimer's disease, parkinson's disease, vaginal cancer, epilepsy Anxiety Disorders, Autoimmune Disease, Back Pain, Back Sprain, Bipolar Disorder, Brain Tumor, Malignant, Bruxism, Bulimia, Cervical Disc Disease, Cardiovascular Disease, Neoplasms , chronic respiratory disease, mental and behavioral disorder, Cystic Fibrosis, Hypertension, Diabetes, Asthma, Autoimmune inflammatory media arthritis ed. chronic kidney disease, inflammatory joint disease, impotence, alcohol spectrum feta, dysthymic disorder, eczema, tuberculosis, chronic fatigue syndrome, constipation, inflammatory bowel disease, lupus disease, mouth ulcer, mouth cancer, body pain, fever, hepatitis ABC, syphilis, diarrhea, HIV / AIDS, Huntington's disease, back acne, chronic kidney failure, addison's disease, chronic pain, Crohn's pain, cystic fibrosis, fibromyalgia, inflammatory Bowel disease, fungal nail disease, Lyme disease, Celia disease, Lymphoma, Major depression, Malignant melanoma, Mania, Melorheostosis, Meniere's disease, Mucopolysaccharidosis, Multiple sclerosis, Muscular dystrophy, Rheumatoid arthritis. You can reach him Email Via drimolaherbalmademedicine@gmail.com / whatsapp +2347081986098    Website/ www.drimolaherbalmademedicine.wordpress.com

    ReplyDelete