Thursday, March 26, 2009

Nywele na Ngono

Nywele na Ngono



Nywele ni sehemu muhimu sana ya urembo wa mwanamke kama ilivyo sehemu nyingine za mwili wake na wakati huohuo nywele hizo zinachukua nafasi kubwa ktk mapenzi na huongeza raha na mvuto kwa mpenzi wako hasa kama mnatoana jasho wakati mnafanya mapenzi.


Nywele za mwanamke hupendeza zaidi machoni kwa mwanaume/mpenzi wako mara baada ya kufanya mapenzi kuliko zinavyokuwa mara baada ya kutoka kwa “hairdresser/Salon”, mwanaume hufurahia kucheza na kichwa cha mwanamke na kuhisi ule mkwaruzo wa nywele, harufu yake asilia iliyochanganyikana na mafuta, sabuni au “shampoo” (hivyo hakikisha hupaki mafuta yenye harufu kali kichwani).

Inasemekana wanaume wengi hupenda kushika kichwa cha mwanamke wakati wa kufanya mapenzi au kuchezeana na hukosa raha fulani ikiwa watawekewe mipaka kuwa wasiguse kichwa kwa vile wataharibu mtindo wa nywele uliogharamia “Salon”.

Sina shaka umeshawahi kusikia baadhi ya wanaume wakilalamika kuwa hawapendi wake/wapenzi wao wavae “wigs” kitandani kwa vile wanashindwa kucheza na vichwa vyao, sina hakika na wale wanawake wanaoondoa nywele zote kichwani.

Mwanamke na nywele.

Si wanawake wote wanavutiwa na nywele za vichwani mwa wanaume bali huvutiwa na nywele sehemu nyingine za mwili kama vile kwapani, usoni (nyusi, ndevu n.k ), kifuani, sirini na kwingineko ila nywele ninazozungumzia hapa ni zile za kichwani mwa mwanamke.

Kuna wanawake huvutiwa sana na nywele za usoni (zinawafanya wahisi wako na Real man) na zile za miguuni hasa wakati wanatoa “massage” ya miguu kwa mpenzi, ule mkwaruzo wake huwapa raha ya ajabu inayowafanya wafurahie kufanya wanachokifanya kwa wakati huo ambacho ni kumkanda miguu yake, vilevile wanapenda kucheza na zile za sirini wakati wanaongea (mara nyingi ni baada yakufanya mapenzi).


Ngono ni sanaa

No comments:

Post a Comment