Showing posts with label mapenzi. Show all posts
Showing posts with label mapenzi. Show all posts

Friday, October 25, 2013

Matatizo ya kufanya mapenzi

kukosa hamu ya kufanya mapenzi
Matatizo ya kufanya mapenzi au kujamiana kwa wanawake yanatambulika kama tatizo linalojirudia kwa muda mrefu ambapo huathiri mzunguko wa tendo la kujamiana (kusisimka, kufikia kilele, kurudia) na hivyo kusababisha msongo wa mawazo au kuharibu uhusiano wa mwanamke na mpendwa wake. Tatizo hili huathiri asilimia 43 ya wanawake wa rika zote duniani na huonekana sana kwa wanawake wenye umri kati ya 45-64.
Visababishi vya tatizo hili kwa wanawake ni;

Endelea Kusoma

Sunday, April 1, 2012

Karibu

Sunday, March 18, 2012

Kupungua au Kukosa Hamu ya Kufanya Mapenzi

kukosa hamu ya kufanya mapenzi
Matatizo ya kufanya mapenzi au kujamiana kwa wanawake yanatambulika kama tatizo linalojirudia kwa muda mrefu ambapo huathiri mzunguko wa tendo la kujamiana (kusisimka, kufikia kilele, kurudia) na hivyo kusababisha msongo wa mawazo au kuharibu uhusiano wa mwanamke na mpendwa wake. Tatizo hili huathiri asilimia 43 ya wanawake wa rika zote duniani na huonekana sana kwa wanawake wenye umri kati ya 45-64.
Visababishi vya tatizo hili kwa wanawake ni;
  • Msongo wa mawazo – Asilimia kubwa ya tatizo hili linaweza kutokea kutokana na msongo wa mawazo ambapo huchangiwa na ugumu wa maisha (uchumi), matatizo katika uhusiano (ugomvi, kutoelewana, kutoaminiana au kukosa uaminifu katika uhusiano {infedility} nk) na magonjwa mbalimbali.
  • Kupungua au kukosekana upendo/mapenzi katika uhusiano au ndoa
  • Kujifungua mtoto – Hii ni kutokana na homoni aina ya prolactin kuwa katika kiwango cha juu wakati mama ananyonyesha, homoni hii pia hufanya kazi ya kumfanya mtu kuridhika baada ya tendo la ndoa/kujamiana kwa kuingiliana na ufanyaji kazi wa homoni/kichocheo chengine kinachojulikana kama dopamine (ambayo ndio humfanya mtu kufikia kilele wakati wa kujamiana). Mbali na kunyonyesha, homoni ya prolactin pia huongezeka wakati mtu amelala (usingizi mzito au REM sleep), wakati wa alfajiri, baada ya kufanya mazoezi, kula,baada ya tendo la kujamiana, baada ya upasuaji mdogo na hata baada ya kupata degedege. Sababu nyengine ya kuongezeka kiwango cha kichocheo hiki cha prolactin ni kuwa na saratani katika ubongo (anterior pitituary tumors). Dalili za saratani hii ni pamoja na kutonyonyesha vizuri kwa mama, kukosa hedhi, ugumba kwa wanawake na uhanithi kwa wanaume (impotence).
  • Kupungua mzunguko wa damu katika tupu ya mwanamke na hivyo kusababisha maumivu wakati wa kujamiana.
  • Hypothyroidism – Matatizo ya homoni ya tezi la koo, huonekana sana kwa wanawake kuliko wanaume.
  • Utumiaji wa vidonge vya kupanga uzazi au vya majira kwa muda mrefu
  • Unywaji pombe kupindukia – Kinyume na fikira potofu za watu wengi ambao huamini kwamba unywaji pombe kali huongeza hamu ya kujamiana au kupunguza uzito lakini ukweli ni kwamba pombe kali au kilevi cha aina yoyote hupunguza hamu ya kujamiana na pombe huongeza uzito na kusababisha utapia mlo.
  • Ugonjwa wa kisukari
  • Uvutaji sigara
  • Ujauzito – Kutokana na mabadiliko katika mfumo wa homoni au vichocheo wakati wa ujauzito, na pia kutokana na mabadiliko ya maumbile ya wanawake wakati huu na hivyo kuchangia kutojiamini kwa mwanamke.
  • Uzito uliopitiliza (obesity)
  • Ugonjwa wa mifupa (arthritis)
  • Utumiaji madawa ya kulevya
  • Madhara katika neva inayohusika na kuongeza msisimko wakati wa kujamiana (pudendal nerve damage) wakati wa upasuaji wa kuondoa mfuko wa uzazi kwa mwanamke mwenye matatizo ya uzazi au katika mfuko wa kizazi.
  • Madhara ya dawa – Kama dawa za kutibu shinikizo la damu, antidepressant medication, dawa za saratani nk.
  • Uchovu – Kuzidiwa kwa mwanamke na majukumu ya kulea mtoto/watoto, kazi na kumhudumia mume wake hivyo kusababisha uchovu.
  • Ugonjwa wa moyo
  • Saratani ya aina yoyote ile
  • Kuwa na wasiwasi (anxiety), depression nk.
  • Historia ya kubakwa, au kupata maumivu wakati wa kujamiana hapo awali kutokana na mwanamke kutokuwa tayari kujamiana au kutotayarishwa vyema kabla ya kujamiana au magonjwa ya zinaa.
  • Tatizo la vaginismus – Hii ni tatizo ambalo husababisha tupu ya mwanamke kuwa ndogo wakati wa kujamiana na hivyo husababisha mwanamke kupata maumivu wakati wa kujamiana.
  • Kupenda inataneti kupita kiasi (addiction) – Katika tafiti mpya iliyofanyika mwaka huu nchini marekani, imeonyesha ya kwamba kati ya ndoa 6,000 zilizovunjika asilimia 57 zimesababishwa na mwenza mmoja au wote kupenda kuchat au kutumia intaneti kupita kiasi na hivyo kusababishwa msisimko kupotea kati ya wenza wawili na hatimaye mwisho ni kupungua uwezo au hamu ya kujamiana.
Ni kundi gani la wanawake lililo katika hatari ya kukumbwa na tatizo hili?

  • Wanawake ambao wana historia ya kupungua hamu ya kujamiana
  • Wale ambao wamefanyiwa upasuaji wa kuondoa mayai yao ya uzazi kutokana na sababu mbalimbali
  • Wanawake ambao waliofika umri wa kuacha kupata hedhi (menopause- miaka 42-58)) na kupata dalili mbalimbali kama kutokwa na jasho usiku, kukosa usingizi mzuri na depression.
Kwa wanaume, visababishi vya tatizo la kupungua hamu au uwezo wa kujamiana ni kama ifuatavyo;
  • Msongo wa mawazo kama nilivyoeleza hapo juu
  • Kupungua au kukosekana upendo/mapenzi katika uhusiano/ndoa
  • Unywaji pombe kupindukia kama nilivyoeleza awali
  • Utumiaji wa dawa za kulevya
  • Uvutaji sigara – Hupunguza kiwango na uzito wa shahawa kwa wanaume. Uzito wa shahawa (concentration of spermatozoa in semen) hupungua kwa asilimia 22-57 kwa wale wanaovuta sigara. Uwezo wa shahawa kuogelea kwenye mirija ya uzazi ya mwanamke pia nao hupungua kwa asilimia 20 kwa wale wanaovuta sigara ikilinganishwa na wale wanaume wasiovuta sigara.
Tafiti nyengine zimethibitisha kuwa wanaume wanaovuta sigara wana asilimia kubwa ya kutoa shahawa ambazo hazina maumbile mazuri au ya kawaida na hivyo kuongeza uwezekano wa mimba kutoka (spontaneous abortion) au kuzaa mtoto mwenye maumbile ambayo sio ya kawaida (birth defects). Tafiti mbalimbali pia zimethibitisha kuwa uvutaji sigara huharibu mirija ya seminiferous tubules ambayo hupatikana kwenye korodani na ni sehemu ambapo shahawa hutengenezwa, hivyo uharibifu wake hupunguza wingi na uzito wa shahawa.
Pia uvutaji sigara hupunguza vichocheo aina ya testerone, growth hormone, na nk.Wanaume wenye kiwango kidogo cha testerone huwa na tatizo la kupungukiwa uwezo wa kujamiana na kiwango kidogo cha shahawa.Uvutaji sigara hupunguza mzunguko wa damu unaopita/kwenda kwenye moyo na kwenye uume na hivyo basi kumfanya mwanamume kushindwa kusimika na kupata tatizo la kupungua uwezo wa kujamiana (vascular impotence).
Katika tafiti zilizofanyika, asilimia 97 ya wale waliogunduliwa na tatizo la vascular impotence walikuwa wavutaji sigara na katika tafiti nyengine asilimia 87 ya wale wenye tatizo hili la vascular impotence walikuwa pia wavutaji sigara. Katika tafiti iliyohusisha wapenzi 290 hapo mwaka 1999, ilionyesha ya kwamba wanaume ambao walikuwa wavutaji sigara walifanya tendo la ndoa na wake zao mara 6 tu kwa mwezi mzima na wale ambao hawakuwa wavutaji sigara walifanya tendo la ndoa mara mbili zaidi ya wale wavutaji sigara.
Uvutaji sigara, huusishwa pia na kuongezeka kwa chembechembe nyeupe za damu kwenye shahawa ambazo kwa kawaida hutolewa kukiwa na ugonjwa ndani ya mwili, chembechembe hizi ambazo zinakuwepo kwa wingi kwenye shahawa pasi na kuwepo kwa ugonjwa, hupunguza uwezo wa shahawa kuingia na kuungana na yai (ovum) kutoka kwa mwanamke na hivyo kusababisha kutotunga kwa mimba.
  • Ugonjwa wa kisukari
  • Uzito uliopitiliza (obesity) – Kutokana na kuongezeka kwa mafuta ambayo husababisha mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo na uume kuwa midogo na kupungua uwezo wa kujamiana. Kupungua uwezo wa kujamiana au kufanya mapenzi kwa wanaume ni ishara mojawapo ya ugonjwa wa moyo na kiharusi.
  • Hypothyroidism – Matatizo ya vichocheo katika tezi la koo
  • Kuwa na wasiwasi (anxiety), depression
  • Kupenda mambo ya intaneti kupita kiasi (addiction to internet) kama nilivyoeleza awali.
  • Umri – Kuanzia miaka ya 40,kiwango cha kichocheo aina ya prolactin huongezeka na kusababisha kuongezeka kwa kichocheo chengine aina ya dihydro-testerone ambacho husababisha tezi dume kuongezeka na hatimaye kupunguza uwezo wa kusimika kwa mwanamume (rudia makala ya kuvimba tezi dume – Benign Prostate Hyperplasia, BPH)
  • Madhara katika neva inayohusika na kusimika kwa uume (pudendal nerve damage)
  • Kuendesha baiskeli muda mrefu (kwa kipindi kimoja) – Hii hugandamiza neva na mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye uume na kusababisha tatizo la kupungua kwa uwezo wa kusimika kwa mwanamume kwa muda tu (temporary).
Vipimo vya uchunguzi
Kabla ya kufanya vipimo vya uchunguzi, Daktari atachukua historia ya mgonjwa inayohusisha matumizi ya dawa aina mbalimbali, historia ya magonjwa, pamoja na kuangalia dalili za magonjwa mbalimbali. Vipimo vya uchunguzi vitatokana na historia ya mgonjwa ambayo Daktari ameweza kuipata kutoka kwake. Vipimo hivyo vinaweza kuwa
  • Kuangalia magonjwa kwenye tupu ya mwanamke au kama kuna bakteria aina yoyote.
  • – Kuangalia magonjwa ya zinaa
  • Vipimo vya mkojo (urinalysis)
  • Kipimo cha kuangalia mabadiliko yoyote kwenye tupu ya mwanamke (physical changes, thinning of genital tissues, decreased skin elasticity and scarring)
  • Kumpima mgonjwa akili ili kuweza kutambua kiini cha tatizo
  • Vipimo vya vichocheo kama T3, T4, testerone level, growth hormone, prolactin hormone nk.
  • Semen analysis – Kipimo cha kuangalia shahawa, wingi wake (volume), kiwango chake, mvutano wake (liquefaction time), sperm count, maumbile yake (sperm morphology), PH yake, uwezo wake wa kuogelea (sperm motility), kiwango cha sukari na chembechembe nyeupe za damu.
  • BMI – Kipimo cha kuangalia kama mtu anauzito unaolingana na urefu wake pamoja na umri wake au ana uzito uliopitiliza
  • Vipimo vya ugonjwa wa shinikizo la damu – Kwa wale wenye shinikizo la damu au dalili zake au wanaotumia dawa za shinikizo la damu
  • Vipimo vya ugonjwa wa kisukari – Fasting Blood Glucose test, Oral Glucose Tolerance Test (OGTT), glycosylated hemoglobin (Hb A1C) rudia makala ya Kisukari kwenye tovuti ya Tanzmed.
Tiba ya tatizo hili
Tiba ya tatizo hili inahusisha
1.Kubadilisha mfumo wa maisha
  • Kufanya mazoezi mara kwa mara – Mazoezi huongeza stamina, hupunguza uzito,humfanya mtu kuwa na umbile zuri, furaha na kuongeza ufanisi wakati wa kujamiana
  • Kupunguza msongo wa mawazo kwa kukubali kwamba tatizo lipo baina ya wanandoa na hivyo kutafuta suluhu pamoja na kuacha ugomvi. Matatizo ya kimaisha (fedha, nk) lazima yatafutiwe ufumbuzi.Kufanya mazoezi ya pelvic muscles kwa kufanya kama unazuia mkojo wakati unahisi haja ndogo na kuhesabu kutoka moja hadi tano, baada ya tano pumzika na halafu rudia. Haya mazoezi (kegel exercise) huongeza uwezo wa kujamiana kwa wanawake
2. Kubadilisha mfumo wa maisha kwa wapenzi
  • Zungumza na mwenza wako – Malumbano na matatizo ni vitu vya kawaida katika uhusiano wowote, ni vizuri kwa wenza kukaa pamoja na kuzungumza matatizo yao, kuwa wakweli, waaminifu, kuaminiana, kujaliana na kuzungumza juu ya tendo la ndoa kwa pamoja. Ni vizuri kila mmoja kuainisha vitu anavyopenda na asivyopenda kufanyiwa wakati wa kujamiana. Pale inapotokea mmoja hajapendezwa au kufurahishiwa na uwajibikaji au ufanisi wa mwenzie basi hana budi kutumia lugha nzuri kutafuta kiini cha tatizo na kulitafutia ufumbuzi.
  • Weka mazingira mazuri na muda wa kufanya tendo la ndoa na mwenza wako ili mupate kudumisha uhusiano wenu
  • Ongeza msisimko katika uhusiano wenu kwa kujaribu aina au staili mbalimbali wakati wa kujamiana, kubadilisha muda wa kufanya mapenzi (sio usiku tu hata asubuhi, mchana) au sehemu tofauti na ile muliyoizoea wakati wa kufanya mapenzi (sio kila siku kitandani)
  • Kupata ushauri nasaha kutoka kwa wataalamu wa mambo ya uhusiano, marriage counsellors na hata madaktari wa magonjwa ya akili kwani hawa ni weledi zaidi katika kazi yao.
3.Tiba ya dawa
  • Kutibu ugonjwa ambao ni kiini cha tatizo hili – Kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya zinaa nk.
  • Daktari kumbadilishia mgonjwa dawa zinazoleta madhara kama ya msongo wa mawazo, depression nk.
  • Kutibu tatizo la depression na anxiety
  • Kutumia dawa au jelly zinazolainisha tupu ya mwanamke wakati wa tendo la ndoa kwa wale wanaopata maumivu au kupunguza tupu kuwa kavu au kuwasha (irritation).
  • Tiba ya homoni au vichocheo – Estrogen Replacement Therapy (ERT) and androgen therapy.
  • Dawa aina ya Yohimbine Hydrochloride
4.Vyakula vinavyosaidia kupunguza tatizo hili
Ikumbukwe ya kwamba vyakula hivi sio tiba mbadala bali husaidia tu kupunguza ukubwa wa tatizo hili la kupungua au kukosa hamu ya kufanya mapenzi na kuboresha kwa wale ambao hawana tatizo hili na hivyo kudumisha uhusiano.
  • Kitunguu swaumu – Kitunguu swaumu kina kemikali aina ya allicin ambayo huongeza mzunguko wa damu kwenda kwenye uume, huongeza hamu ya kufanya mapenzi na utolewaji wa shahawa.
  • Habat al soda (black caraway seeds) – Mafuta,mbegu,au unga wa habat soda kama wengi wanavyoita na ambazo zimetumika kwa miaka mingi sana kupunguza tatizo hili na waandishi wengi wameeleza umuhimu wake. Tumia kidogo kwenye chai au maji ya uvuguvugu mara mbili kila siku. Mbegu hizi hupatikana kwa wingi katika nchi za asia kama Saudi Arabia, Syria, Iran, Dubai (UAE), na hata Misri, Tanzania (Dar-es-salaam katika maduka ya dawa za asili ya kariakoo, mbagala, na Zanzibar)
  • Celery au giligilani – Hii huchochea hamu ya tendo la ndoa kutokana na uwepo kwa wingi wa kichocheo aina ya androsterone.
  • Ndizi – kuwepo kwa wingi kwa enzyme aina ya bromelain na madini ya potassium huongezeka msisimko wa kufanya mapenzi kwa wanaume.Potassium pia hupatikana kwenye tikiti maji ambalo pia lina kemikali aina ya arginine ambayo huongeza wingi wa damu katika mishipa ya damu na hivyo kusaidia katika kusimika kwa uume.
  • Parachichi – Huwa na kiwango kikubwa cha folic acid ambayo huvunjavunja protini. Vitamini B6 kwenye parachichi huchochea kutengeza kichocheo aina ya testerone kwa wingi.
  • Mayai – Mayai yana kiwango kikubwa sana cha vitamini aina ya B5 na B6, ambazo husaidia kuleta usawa wa viwango vya vichocheo mwilini na kupunguza msongo wa mawazo.
  • Nyanya/Tungule (tomatoes) – Zina kiwango kikubwa cha virutubisho aina ya bio-active phyto-nutrients, lycopene, na beta carotene ambazo husaidia kuleta damu kwa wingi kwenye uume na hivyo kusaidia kusimika kwa uume
  • Chocolate – Ina kiwango kikubwa cha kemikali aina ya theobromine na phenylethylamine ambazo huongezeka hamu ya kufanya mapenzi.
  • Vitamin A – Husaidia katika kuweka usawa wa vichocheo vya mapenzi (sexual hormones). Vyakula venye wingi wa vitamin hii ni pamoja na karoti, maini,tikiti maji, spinach, maziwa nk.
  • Vitamin B complex – Huongeza kiwango cha kichocheo cha testerone ambacho husaidia katika kuongeza ufanisi wa tendo la ndoa kwa wanaume na wanawake. Vitamini B complex hupatikana kwa wingi kwenye ndizi, viazi tamu, lentils, mboga za majani, parachichi (avocado), mayai, nyama aina ya tuna, bata mzinga, maini nk.
  • Vitamin C – Tafiti zilizofanywa karibuni zimeonyesha ya kwamba vitamini C inapotumiwa pamoja na vitamini nyengine, husaidia L-enantiomer ya ascorbic acid kudhibiti msongo wa mawazo, wasiwasi (anxiety), utolewaji wa homoni ya prolactin na huongeza mzunguko wa damu pamoja na kutolewa kwa kichocheo cha aina ya oxytocin na hivyo kuongeza ufanisi wa tendo la ndoa. Vyakula venye vitamin C ni ndimu, chungwa, limao, brussels sprouts, mapera, tikiti maji, nyanya, broccoli, kiwi, papai, strawberries, pilipili hoho na pilipili mbuzi nk.
  • Vitamin E – Husaidia kudhibiti matamanio ya mwanamume pamoja na kusimika kwa uume kutokana na uwepo wa vichocheo aina androgens na estrogen ambavyo huchanganyikana na homoni za mayai (ovarian hormones) na testerone. Vyakula venye vitamin E ni pilipili hoho, nyanya, olives, tunda aina ya kiwi, papai, mafuta ya alizeti, karanga nk.
  • Madini ya Zinc – Muhimu katika utengenezaji wa testerone
  • Madini ya selenium – Huongeza uwezo na nguvu ya kufanya mapenzi kwa wanaume.
  • Madini ya magnesium na calciumCalcium ni muhimu katika kusaidia ufanisi wa kufanya mapenzi. Huweka mawasiliano ya karibu kati ya ubongo na tezi zinazotoa vichocheo vya mapenzi pamoja na kusaidia katika ufanyaji kazi wao. Madini ya magnesium husaidia kuondoa madhara ya madini ya calcium katika kusaidia kuhimili kusimika kwa uume. Vyakula venye madini ya calcium ni maziwa, mtindi, cheese, siagi, chungwa, almonds, walnuts, maharage meupe, ice cream, chocolate nk.
  • Cinnamon stick (mdalasini) na Asali (Honey) – Mchanganyiko wa vitu hivi viwili husaidia sana katika kuongeza ufanisi kwa wale wenye tatizo hili. Jinsi ya kuandaa, chukua mdalasini robo na changanya na asali nusu lita kisha weka kwa siku tatu, baada ya siku tatu anza kunywa kwa kutumia kikombe cha kahawa mara tatu kwa siku kwa muda wa wiki mbili (kama utatumia mdalasini nusu basi changanya na asali lita moja).

Maneno ndiyo hubomoa na kujenga uhusiano II

Maneno ndiyo hubomoa na kujenga uhusiano.

Hatari iliyopo ni kuwa wanaume wengi wanapowazoea wapenzi wao, hushindwa kutamka neno hilo lakini mwanamke hupenda kusikia akiambiwa hivyo.

Mwambie mpenzi wako jinsi unavyompenda, mthibitishie kuwa mapenzi yako kwake ni makubwa kupita kiasi.

VIPI KUHUSU WANAUME?


Wanawake wengi hulalamika kuwa wanaume ni watata kwenye mapenzi.

Hulaumu kwamba ni ngumu kubaini vitu ambavyo wanaume huhitaji kutoka kwa wanawake.

Wanadai kuwa wakati mwingine hujitahidi kadiri ya uwezo wao kuhakikisha wanawapa furaha lakini wanaume huwa hawana hata msisimko.

Hapa chini, nimekuandalia vitu ambavyo wanaume huhitaji kwa wanawake wao. Moja kwa moja, mambo yakienda chanya huwa ni zaidi ya chombezo na hupagawa.

MAPENZI (Love)
Siku zote wanaume huangalia mapenzi kwa wenzi wao.

Mara nyingi wanaume huwa wepesi kuonesha mapenzi kwa wanawake wao lakini ndani ya nafsi zao, hutegemea mambo mengi kama malipo (return) ya upendo waliotoa kabla.
Wanapenda, kwa hiyo nao huhitaji kupendwa ili waone mambo yanakwenda sawa.

Wanawake wengi huwa wanaficha hisia za kupenda, hili huwaumiza wenzi wao.

Onesha mabadiliko, muoneshe jinsi unavyoridhishwa na upendo wake kisha mtamkie kwamba kwake umefika, halafu thibitisha hilo kwa vitendo.

MVUTO (Attractiveness)
Wanaume huhitaji wapenzi wao wawe na mvuto. Hii inawezekana isiwe na maana kwa wanawake kwa kushindwa kutambua mvuto wao, unavyoweza kuwa kibwagizo murua cha mapenzi.
Vaa vizuri upendeze, hakikisha muda wote unakuwa nadhifu.

Muonekano wako ndiyo utamfanya mwenzi wako ajiamini popote.

Kwa hiyo, kupendeza kwako ni bonge la chombezo kwa mwenzio.

UAMINIFU (Trustful)
Wanaume hupenda wanawake wenye uaminifu wa asilimia 100.

Mwanaume huhitaji mwanamke ambaye muda wote atakuwepo kwa ajili yake kimapenzi, kubadilishana mawazo na kumshirikisha katika siri za maisha yake.

Bahati mbaya wapo wanawake wengi ambao hawana uaminifu hata chembe.

Hilo huwafanya wanaume kukosa imani kwa wapenzi wao.

Jiamini kisha uwe muaminifu.

Mfanye mpenzi wako asikutilie shaka ya aina yoyote kisha uone jinsi maisha yanavyoweza kusonga mbele.

FAMILIA (Family)
Wazo la kila mwanaume anapopata mwanamke, hufikiria ajenge naye familia haraka iwezekanavyo. Hivyo basi, huhitaji mwanamke ambaye yupo tayari kwa hilo.

Kitu ambacho huwakera wengi ni pale wanapokutana na mtu aliye na mawazo ya kurukaruka.

Kama umeshaolewa, muoneshe mumeo jinsi ulivyo fundi wa kuiweka familia pamoja.

Ukifanya hivyo, utakuwa umempatia, kwani hakuna jambo ambalo wanaume huwa hawapendi kama kuona familia inasambaratika.

UKARIMU (Kindness)
Wanaume huwa na matarajio ya kuwaona wanawake wao wakiwa wapole, waungwana na wakarimu. Jitazame na ujitengeneze kuwa hivyo ili umvutie mwenzi wako.

Ukorofi, ubishi na roho mbaya siyo sifa ya kike.

UCHESHI (Funny)
Wanaume hupenda wanawake wanaojua kucheka. Akiwa naye, wazungumze na wacheke. Wanaume huwachukia wanawake wanaopenda kununa. Kama una tabia hiyo, jirekebishe ili umkune mwenzi wako.

U-MWANAMKE (Femaleness)
Kwa kawaida, wanaume hupenda wanawake ambao wanajitambua kuwa wao ni wanawake.

Huwachukia wale wanaojipa sifa ya u-dume au wababe, wanaopenda kutoa amri.

Huhitaji wanawake wanaotimiza wajibu wao kama wanawake kulingana na jamii inavyotambua. Hupenda wanawake wanaojali, kujiheshimu na kadhalika.

Wale walevi hukosa sifa ya u-mwanamke ambayo wanaume huihitaji.

Maneno ndiyo hubomoa na kujenga uhusiano II

Maneno ndiyo hubomoa na kujenga uhusiano.

Hatari iliyopo ni kuwa wanaume wengi wanapowazoea wapenzi wao, hushindwa kutamka neno hilo lakini mwanamke hupenda kusikia akiambiwa hivyo.

Mwambie mpenzi wako jinsi unavyompenda, mthibitishie kuwa mapenzi yako kwake ni makubwa kupita kiasi.

VIPI KUHUSU WANAUME?


Wanawake wengi hulalamika kuwa wanaume ni watata kwenye mapenzi.

Hulaumu kwamba ni ngumu kubaini vitu ambavyo wanaume huhitaji kutoka kwa wanawake.

Wanadai kuwa wakati mwingine hujitahidi kadiri ya uwezo wao kuhakikisha wanawapa furaha lakini wanaume huwa hawana hata msisimko.

Hapa chini, nimekuandalia vitu ambavyo wanaume huhitaji kwa wanawake wao. Moja kwa moja, mambo yakienda chanya huwa ni zaidi ya chombezo na hupagawa.

MAPENZI (Love)
Siku zote wanaume huangalia mapenzi kwa wenzi wao.

Mara nyingi wanaume huwa wepesi kuonesha mapenzi kwa wanawake wao lakini ndani ya nafsi zao, hutegemea mambo mengi kama malipo (return) ya upendo waliotoa kabla.
Wanapenda, kwa hiyo nao huhitaji kupendwa ili waone mambo yanakwenda sawa.

Wanawake wengi huwa wanaficha hisia za kupenda, hili huwaumiza wenzi wao.

Onesha mabadiliko, muoneshe jinsi unavyoridhishwa na upendo wake kisha mtamkie kwamba kwake umefika, halafu thibitisha hilo kwa vitendo.

MVUTO (Attractiveness)
Wanaume huhitaji wapenzi wao wawe na mvuto. Hii inawezekana isiwe na maana kwa wanawake kwa kushindwa kutambua mvuto wao, unavyoweza kuwa kibwagizo murua cha mapenzi.
Vaa vizuri upendeze, hakikisha muda wote unakuwa nadhifu.

Muonekano wako ndiyo utamfanya mwenzi wako ajiamini popote.

Kwa hiyo, kupendeza kwako ni bonge la chombezo kwa mwenzio.

UAMINIFU (Trustful)
Wanaume hupenda wanawake wenye uaminifu wa asilimia 100.

Mwanaume huhitaji mwanamke ambaye muda wote atakuwepo kwa ajili yake kimapenzi, kubadilishana mawazo na kumshirikisha katika siri za maisha yake.

Bahati mbaya wapo wanawake wengi ambao hawana uaminifu hata chembe.

Hilo huwafanya wanaume kukosa imani kwa wapenzi wao.

Jiamini kisha uwe muaminifu.

Mfanye mpenzi wako asikutilie shaka ya aina yoyote kisha uone jinsi maisha yanavyoweza kusonga mbele.

FAMILIA (Family)
Wazo la kila mwanaume anapopata mwanamke, hufikiria ajenge naye familia haraka iwezekanavyo. Hivyo basi, huhitaji mwanamke ambaye yupo tayari kwa hilo.

Kitu ambacho huwakera wengi ni pale wanapokutana na mtu aliye na mawazo ya kurukaruka.

Kama umeshaolewa, muoneshe mumeo jinsi ulivyo fundi wa kuiweka familia pamoja.

Ukifanya hivyo, utakuwa umempatia, kwani hakuna jambo ambalo wanaume huwa hawapendi kama kuona familia inasambaratika.

UKARIMU (Kindness)
Wanaume huwa na matarajio ya kuwaona wanawake wao wakiwa wapole, waungwana na wakarimu. Jitazame na ujitengeneze kuwa hivyo ili umvutie mwenzi wako.

Ukorofi, ubishi na roho mbaya siyo sifa ya kike.

UCHESHI (Funny)
Wanaume hupenda wanawake wanaojua kucheka. Akiwa naye, wazungumze na wacheke. Wanaume huwachukia wanawake wanaopenda kununa. Kama una tabia hiyo, jirekebishe ili umkune mwenzi wako.

U-MWANAMKE (Femaleness)
Kwa kawaida, wanaume hupenda wanawake ambao wanajitambua kuwa wao ni wanawake.

Huwachukia wale wanaojipa sifa ya u-dume au wababe, wanaopenda kutoa amri.

Huhitaji wanawake wanaotimiza wajibu wao kama wanawake kulingana na jamii inavyotambua. Hupenda wanawake wanaojali, kujiheshimu na kadhalika.

Wale walevi hukosa sifa ya u-mwanamke ambayo wanaume huihitaji.

‘Kumshika’ mpenzi wako siyo mpaka umpe mapenzi kinyume na maumbile!

“Mwanaume gani usiyeridhika na mapenzi ninayokupa…? Nimefikia hatua ya kukupa hata mapenzi kinyume na maumbile ili usitoke nje lakini bado, hivi ni kipi ulichokikosa kwangu?” alisikika akipayuka mwanamke huyo.

Maneno aliyokuwa akiyatoa yule mwanamke yalinichoma sana. Nikabaini siri moja ambayo nahisi ipo kwa wanawake wengi walio kwenye ndoa na hata wale walio kwenye uhusiano wa kawaida kwamba, wanafikia hatua ya kutoa aina hiyo ya penzi eti ili wapenzi wao wasiwasaliti. Jamani hii inaingia akilini kweli?


Unafikia hatua ya kuhatarisha maisha yako kisa unataka kukamilisha ile sentesi ya kwamba unampa mumeo kila anachokitaka? Huo ni ulimbukeni na kama wapo wanaoendelea kufanya hivyo, wanajitafutia matatizo yatakayowafanya waje kujuta baadaye.


Ni kweli washauri wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa, ili uweze kumshika vilivyo mpenzi wako unatakiwa kuhakikisha unampatiliza katika kila anachokitaka lakini hawakuzungumzia ishu ya wewe kukubali mapenzi kinyume na maumbile. Hawakurusu hilo kwa kuwa wanajua madhara ya kufanya hivyo. Sasa iweje leo ukubali kufanya dhambi hiyo eti kwa kuwa mpenzi wako kataka na unampenda?
Katika ulimwengu wa sasa wapo wanaume wa ajabu sana. Hawa ni wale ambao si wastaarabu. Wao hawaangalii madhara yanayoweza kuwapata wenzao bali wanaangalia kujifurahisha wao tu. Mbaya zaidi baadhi ya wanawake nao wamekuwa mbumbumbu.
Eti kwa kuogopa kuachwa au kusalitiwa wanasema bora wafanye hivyo. Jamani, ifike wakati tufikirie kila tunalolifanya katika maisha yetu ya kila siku. Zipo mbinu nyingi za kumridhisha mpenzi wako na wala asifikirie kukuacha wala kukusaliti bila hata kumkubalia afanye hivyo.
Pia unatakiwa kufahamu kwamba, unaweza kumpa mpenzi/mume wako mapenzi hayo lakini bado akakusaliti tu. Sasa kwa nini ujidhalilishe?

Ni kamchezo ka’ nyumba ndogo


Ukijaribu kuchunguza utabaini kuwa wanaoongoza kwa mchezo huo mchafu ni wale wezi wa mapenzi ambao hufahamika kwa jina la nyumba ndogo.
Hawa eti wanatumia mbinu hiyo kuwashika waume za watu. Kimsingi hii ni aibu na wanaokubali kufanyiwa hivyo wanajidhalilisha na hawawezi kudumu na wanaume wao.

Usithubutu kabisa


Mapenzi kinyume na maumbile licha ya kwamba yamekatazwa hata na vitabu vitakatifu, madhara yake kiafya pia ni makubwa. Wapo wengi ambao sasa wanajuta kwa kufanya mchezo huo kutokana na kupata matatizo wakati wa kujifungua lakini pia wengi wao imekuwa ni rahisi kuambukizwa magonjwa mbalimbali ya zinaa ukiwemo Ukimwi.

Ni laana


Wanaofanya hivyo wamelaaniwa na wanaweza kushangaa uhusiano wao unakumbwa na matatizo kisha kusambaratika kwani Mungu hawezi kuubariki ule unaokwenda kinyume na maagizo yake.
Ni suala tu la kukaa na kujiuliza, wewe mwanamke unapata raha gani kufanya mapenzi kwa njia ambayo haijaruhusiwa? Wakati mwingine nashindwa hata kuwaelewa hawa wanaofikia hatua ya kujisifia kuwa eti wanawaachia waume zao ‘wajisevie’ wanachotaka kwa kuwa wanawapenda.
Hivi watakuwa na akili timamu? Kumpenda mtu ndiyo uwe tayari kuhatarisha maisha yako kiasi hicho? Tena kwa taarifa yako wale wanaowakubalia wapenzi wao mapenzi kunyume na maumbile wanaonekana wajinga na wanadharaulika. Hakuna mwanaume anayeweza kumheshimu mwanamke anayeweza kuuweka rehani mwili wake kwa njia hiyo.
Nimalizie makala haya kwa kusema kuwa, kanuni ya kwamba unatakiwa kuhakikisha unampatia mpenzi wako kile anachokipenda inabaki palepale lakini umkubalie katika yake yasiyo na madhara kwako. Yale ambayo unaona yatakuletea matatizo, mkatalie kwa kumpa sababu za msingi. Kama ni muelewa atakuelewa, asipokuelewa kuwa tayari akuache lakini usihatarishe maisha yako.

‘Kumshika’ mpenzi wako siyo mpaka umpe mapenzi kinyume na maumbile!

“Mwanaume gani usiyeridhika na mapenzi ninayokupa…? Nimefikia hatua ya kukupa hata mapenzi kinyume na maumbile ili usitoke nje lakini bado, hivi ni kipi ulichokikosa kwangu?” alisikika akipayuka mwanamke huyo.

Maneno aliyokuwa akiyatoa yule mwanamke yalinichoma sana. Nikabaini siri moja ambayo nahisi ipo kwa wanawake wengi walio kwenye ndoa na hata wale walio kwenye uhusiano wa kawaida kwamba, wanafikia hatua ya kutoa aina hiyo ya penzi eti ili wapenzi wao wasiwasaliti. Jamani hii inaingia akilini kweli?


Unafikia hatua ya kuhatarisha maisha yako kisa unataka kukamilisha ile sentesi ya kwamba unampa mumeo kila anachokitaka? Huo ni ulimbukeni na kama wapo wanaoendelea kufanya hivyo, wanajitafutia matatizo yatakayowafanya waje kujuta baadaye.


Ni kweli washauri wa masuala ya mapenzi wanaeleza kuwa, ili uweze kumshika vilivyo mpenzi wako unatakiwa kuhakikisha unampatiliza katika kila anachokitaka lakini hawakuzungumzia ishu ya wewe kukubali mapenzi kinyume na maumbile. Hawakurusu hilo kwa kuwa wanajua madhara ya kufanya hivyo. Sasa iweje leo ukubali kufanya dhambi hiyo eti kwa kuwa mpenzi wako kataka na unampenda?
Katika ulimwengu wa sasa wapo wanaume wa ajabu sana. Hawa ni wale ambao si wastaarabu. Wao hawaangalii madhara yanayoweza kuwapata wenzao bali wanaangalia kujifurahisha wao tu. Mbaya zaidi baadhi ya wanawake nao wamekuwa mbumbumbu.
Eti kwa kuogopa kuachwa au kusalitiwa wanasema bora wafanye hivyo. Jamani, ifike wakati tufikirie kila tunalolifanya katika maisha yetu ya kila siku. Zipo mbinu nyingi za kumridhisha mpenzi wako na wala asifikirie kukuacha wala kukusaliti bila hata kumkubalia afanye hivyo.
Pia unatakiwa kufahamu kwamba, unaweza kumpa mpenzi/mume wako mapenzi hayo lakini bado akakusaliti tu. Sasa kwa nini ujidhalilishe?

Ni kamchezo ka’ nyumba ndogo


Ukijaribu kuchunguza utabaini kuwa wanaoongoza kwa mchezo huo mchafu ni wale wezi wa mapenzi ambao hufahamika kwa jina la nyumba ndogo.
Hawa eti wanatumia mbinu hiyo kuwashika waume za watu. Kimsingi hii ni aibu na wanaokubali kufanyiwa hivyo wanajidhalilisha na hawawezi kudumu na wanaume wao.

Usithubutu kabisa


Mapenzi kinyume na maumbile licha ya kwamba yamekatazwa hata na vitabu vitakatifu, madhara yake kiafya pia ni makubwa. Wapo wengi ambao sasa wanajuta kwa kufanya mchezo huo kutokana na kupata matatizo wakati wa kujifungua lakini pia wengi wao imekuwa ni rahisi kuambukizwa magonjwa mbalimbali ya zinaa ukiwemo Ukimwi.

Ni laana


Wanaofanya hivyo wamelaaniwa na wanaweza kushangaa uhusiano wao unakumbwa na matatizo kisha kusambaratika kwani Mungu hawezi kuubariki ule unaokwenda kinyume na maagizo yake.
Ni suala tu la kukaa na kujiuliza, wewe mwanamke unapata raha gani kufanya mapenzi kwa njia ambayo haijaruhusiwa? Wakati mwingine nashindwa hata kuwaelewa hawa wanaofikia hatua ya kujisifia kuwa eti wanawaachia waume zao ‘wajisevie’ wanachotaka kwa kuwa wanawapenda.
Hivi watakuwa na akili timamu? Kumpenda mtu ndiyo uwe tayari kuhatarisha maisha yako kiasi hicho? Tena kwa taarifa yako wale wanaowakubalia wapenzi wao mapenzi kunyume na maumbile wanaonekana wajinga na wanadharaulika. Hakuna mwanaume anayeweza kumheshimu mwanamke anayeweza kuuweka rehani mwili wake kwa njia hiyo.
Nimalizie makala haya kwa kusema kuwa, kanuni ya kwamba unatakiwa kuhakikisha unampatia mpenzi wako kile anachokipenda inabaki palepale lakini umkubalie katika yake yasiyo na madhara kwako. Yale ambayo unaona yatakuletea matatizo, mkatalie kwa kumpa sababu za msingi. Kama ni muelewa atakuelewa, asipokuelewa kuwa tayari akuache lakini usihatarishe maisha yako.

Usiusaliti moyo wako

Leo nataka tuzungumzie kiapo mwanzo wa uhusiano, ambapo wengi hawakifahamu au hawajui kinatumika wakati gani. Wengi wamevunja viapo vya mapenzi na kujikuta wakigeuka mateso kwa wenzao.

Siku zote mapenzi ni mkataba wa watu wawili waliokubaliana kuwa kitu kimoja kuishi katika hali ya shida na raha. Wapendanao wa kweli huishi katika mkataba ambao mmoja akienda kinyume huwa msaliti.

Mapenzi ya wawili ni mkataba wa makubaliano ambayo hutengeneza katiba inayokuwa muongozo katika uhusiano wao.

Mnapoanza mapenzi kila mtu huukubali mkataba huo na kuahidi ataulinda kwa nguvu zake zote, nguzo kuu za makubaliano huwa ni uaminifu, tabia nzuri, huruma upendo na uvulivu. Tuangalie kitu kimojakimoja ndani ya mkataba huo:

UAMINIFU: Mpaka mnaamua kuwa mwili mmoja ina maana mmekubali kwa ridhaa yenu. Mmewaacha wengi na kuamua kuwa pamoja hivyo mnatakiwa kulilinda penzi lenu kwa kuwa waaminifu. Mmoja wenu akisaliti ni lazima kuvuruga penzi.

TABIA NZURI: Ndiyo inayobeba uwakilishi wa mwanadamu ndani ya nyumba, ni nguzo imara ambayo itakufanya usimame popote kwa kujiamini. Wengi hukosea wanapojiona wana sura umbile zuri au fedha, hivyo kuanza kuwanyanyasa wenzao kwa kujivunia walivyonavyo wakisahau kuwa hakuna kiumbe kilichoumbwa kwa ajili ya kukasirishwa.

HURUMA: Ndani ya uhusiano huruma ni kitu muhimu sana kwa wapenzi kwa vile ukiwa na huruma huwezi kumuumiza mwenzako. Nyumba yenye huruma kwa wapendanao hudumu milele. Ambaye hana huruma hufanya jambo lolote bila kujali maumivu ya mwenzake.

UPENDO: Huu ndiyo unaobeba kila kitu kwa vile mwenye upendo ana huruma, ni mvumilivu na tabia njema ndiyo asili yake. Wote mkiwa hivyo hata familia yetu itakuwa yenye tabia nzuri kwa vile nao watakuwa sehemu ya upendo kuwapenda wote.
Hapa mara nyingi kumekuwa na tatizo kwa baadhi ya watu kuchagua wachache wa kuwapenda, hasa wanawake wamekuwa na kasumba ya kuchukia ndugu wa mume na mwisho wa siku ndoa huvunjika.

UVUMILIVU: Huu ndiyo muhimu katika maisha yetu ya kila siku, wengi wasio wavumilivu wamekuwa wakitengana na wenzao. Katika maisha ya mwanadamu kuna vitu ambavyo tunatakiwa tuvumiliane kwa vile wanadamu ni viumbe ambao hawajakamilika.

Kukosana ni sehemu ya maisha lazima mvumiliane, mtangulize kusameheana na kuyasahau yaliyopita. Yapo ya kuvumilia, lakini si yaliyovuka mipaka kwa mtu kushindwa kujirekebisha. Mwanadamu mwenye akili timamu ujifunza kutokana na makosa na kuwa tayari kukosolewa na kuomba msamaha anapokosea.

Usiusaliti moyo wako

Leo nataka tuzungumzie kiapo mwanzo wa uhusiano, ambapo wengi hawakifahamu au hawajui kinatumika wakati gani. Wengi wamevunja viapo vya mapenzi na kujikuta wakigeuka mateso kwa wenzao.

Siku zote mapenzi ni mkataba wa watu wawili waliokubaliana kuwa kitu kimoja kuishi katika hali ya shida na raha. Wapendanao wa kweli huishi katika mkataba ambao mmoja akienda kinyume huwa msaliti.

Mapenzi ya wawili ni mkataba wa makubaliano ambayo hutengeneza katiba inayokuwa muongozo katika uhusiano wao.

Mnapoanza mapenzi kila mtu huukubali mkataba huo na kuahidi ataulinda kwa nguvu zake zote, nguzo kuu za makubaliano huwa ni uaminifu, tabia nzuri, huruma upendo na uvulivu. Tuangalie kitu kimojakimoja ndani ya mkataba huo:

UAMINIFU: Mpaka mnaamua kuwa mwili mmoja ina maana mmekubali kwa ridhaa yenu. Mmewaacha wengi na kuamua kuwa pamoja hivyo mnatakiwa kulilinda penzi lenu kwa kuwa waaminifu. Mmoja wenu akisaliti ni lazima kuvuruga penzi.

TABIA NZURI: Ndiyo inayobeba uwakilishi wa mwanadamu ndani ya nyumba, ni nguzo imara ambayo itakufanya usimame popote kwa kujiamini. Wengi hukosea wanapojiona wana sura umbile zuri au fedha, hivyo kuanza kuwanyanyasa wenzao kwa kujivunia walivyonavyo wakisahau kuwa hakuna kiumbe kilichoumbwa kwa ajili ya kukasirishwa.

HURUMA: Ndani ya uhusiano huruma ni kitu muhimu sana kwa wapenzi kwa vile ukiwa na huruma huwezi kumuumiza mwenzako. Nyumba yenye huruma kwa wapendanao hudumu milele. Ambaye hana huruma hufanya jambo lolote bila kujali maumivu ya mwenzake.

UPENDO: Huu ndiyo unaobeba kila kitu kwa vile mwenye upendo ana huruma, ni mvumilivu na tabia njema ndiyo asili yake. Wote mkiwa hivyo hata familia yetu itakuwa yenye tabia nzuri kwa vile nao watakuwa sehemu ya upendo kuwapenda wote.
Hapa mara nyingi kumekuwa na tatizo kwa baadhi ya watu kuchagua wachache wa kuwapenda, hasa wanawake wamekuwa na kasumba ya kuchukia ndugu wa mume na mwisho wa siku ndoa huvunjika.

UVUMILIVU: Huu ndiyo muhimu katika maisha yetu ya kila siku, wengi wasio wavumilivu wamekuwa wakitengana na wenzao. Katika maisha ya mwanadamu kuna vitu ambavyo tunatakiwa tuvumiliane kwa vile wanadamu ni viumbe ambao hawajakamilika.

Kukosana ni sehemu ya maisha lazima mvumiliane, mtangulize kusameheana na kuyasahau yaliyopita. Yapo ya kuvumilia, lakini si yaliyovuka mipaka kwa mtu kushindwa kujirekebisha. Mwanadamu mwenye akili timamu ujifunza kutokana na makosa na kuwa tayari kukosolewa na kuomba msamaha anapokosea.

Unatarajia nini kutoka kwa mchumba wako

Je, ni kweli kwamba ndoa ni furaha tu? Hakuna huzuni? Hakuna ugomvi? Rafiki zangu, hata viongozi wa dini, wanapofungisha ndoa, husisitiza kuhusu kuvumiliana, kutunzana na kupendana kwa dhati hata katika kipindi cha shida na raha.

Kwa bahati mbaya, baada ya rafiki zetu wanapokea tofauti maneno haya, wanaamini kwa kuambiwa, humaanisha kwamba kupendana labda hata kama fedha ya kula itakosekana nyumbani, mwenzake akiumwa n.k. Huo ni mtazamo tasa. Katika mada hii nitakufumbua, ujue nini zaidi utakutana nacho ukiwa ndani ya ndoa.

KWANINI TUNAJADILI?
Rafiki yangu ipo haja ya kujadiliana juu ya jambo hili tena kirafiki kabisa. Haya ni mambo ambayo sisi vijana tunakutana nayo. Ni wazi kwamba, kila kijana anawaza kuhusu ndoa.

Anawaza kuoa au kuolewa. Anatamani kuwa na familia yake ili aitwe mama au baba, au siyo jamani? Sasa kabla ya kuingia kwenye hizo ndoa ni lazima tuzijue kwanza, hii ndiyo sababu hasa iliyonisukuma kuandika mada hii.

FIKRA ZA WENGI
Kama nilivyoeleza hapo juu, fikra za wengi ni tofauti. Asilimia kubwa wanafikiria zaidi kuhusu maisha mazuri yasiyo na mikwaruzano. Wanawaza kufurahia ndoa na kudhani hakuna changamoto nyingine.
Wapo wanaofikiria hata suala la tendo la ndoa. Kwamba watakuwa huru kukutana kila siku kadiri watakavyoweza kwa kuwa wapo pamoja ndani. Hii ni mitazamo mibaya sana katika ndoa.

Ni kweli unaweza kufanya tendo la ndoa na mwenzako mara nyingi uwezavyo, lakini nani amekudanganya kwamba kila siku utaendelea kumuona kama umuonavyo leo? Amini usiamini, zipo ndoa nyingi zinazolalamikia suala la tendo la ndoa.
Kuna ambao wanadai hawatoshelezwi huku wengine wakilalama kuwa wenzi wao hawataki kabisa kutoa unyumba. Unajua kwa nini? Ama ana mtu mwingine pembeni au amechoshwa na mapenzi ya aina moja kila siku.

(i) Wanaume
Hawa fikra zao huwa kwenye suala la usafi, wanaamini wakiwa kwenye ndoa nyumba itakuwa safi, nguo zitafuliwa, kupikiwa na mambo mengine ya kifamilia.
Akili zao zinakomea hapo tu, hawawazi kuhusu migogoro na namna ya kutatua. Wanaota kuwa na maisha mazuri, kuwa na watoto na kujijengea heshima kwa jamii. Hilo tu, basi!

(ii) Wanawake
Baadhi ya hawa ninaowazungumzia hufikiria kuhusu kuvaa vizuri, kutolewa out, kupata watoto na mengineyo. Kamwe hawana muda wa kufikiria juu ya matatizo ambayo yanaweza kutokea katika maisha ya ndoa.
Hili ni tatizo. Rafiki zangu, maisha ya ndoa hayana furaha siku zote. Kuna wakati dhoruba hutokea na kusababisha mifarakano hivyo kuhitajika umakini wa hali ya juu katika kumaliza tatizo. Si kila siku kuna amani.

TATIZO LIPO WAPI?
Kwa wale ambao wana mitazamo ambayo nimeeleza hapo juu, huwa hawana muda kwanza wa kuwachunguza wapenzi wao, lakini pia wao wenyewe kuonesha tabia zao halisi ili wenzi wao waweze kusoma kama wataweza kuendana nao.
Rafiki zangu, kwa ujumla hatutakiwi kufikiria mazuri pekee kwenye ndoa, kuna mengi ya kuvumiliana. Lakini pia kabla ya kuamua kuingia kwenye ndoa na mwenzako, kipengele kifuatacho hapa chini ni silaha muhimu sana kwako.

ISHI MAISHA YAKO HALISI
Huwezi kumjua mwenzako kama atakuwa anaishi kisanii na wewe. Sikiliza, kwa wiki mnakutana mara mbili tu, tena mnakaa kwa muda usiozidi masaa mawili, si rahisi sana kuweza kujuana tabia zenu halisi.

Pamoja na hayo, wataalamu wa mambo ya mapenzi wanashauri ili mwenzi aweze kuwa wazi zaidi kwa mwenzake ni vyema yeye akaanza kuwa wazi na kuishi maisha yake halisi kwa uwazi. Usijilazimishe kupenda kitu ambacho hukipendi. Kama kuna jambo ambalo analifanya na linakuboa, mwambie ajue ukweli.

Kwanza, uwazi wako kwake utamfanya naye awe wazi kwako. Hatakuwa na sababu ya kuigiza maisha wakati wewe unaishi maisha yako halisi.

Kila mmoja akimjua mwenzake, ndoa haiwezi kuwa na matatizo, maana kila mtu atakuwa anajua anaishi na mtu wa aina gani. Inawezekana kabisa, mmoja wenu akaona tabia za mwenzake zimemshinda. Kama ni kweli na umegundua kwamba kuingia kwenye ndoa ni sawa na utumwa, fanya maamuzi!

NATAMANI sana kuona maisha ya vijana wa sasa yakiwa hayana migogoro, hasa ya mapenzi. Ni furaha yangu kuona vijana wakifanikiwa katika kazi zao na maisha yao kwa ujumla. Rafiki zangu, maisha bora au utaratibu mzuri wa maisha unatokana na uhusiano mwema wa mhusika na mwenzake.

Kama ulikuwa hujui, leo chukua hii elimu, kijana/mtu ambaye amegombana na mpenzi wake usiku uliopita, siku yake huwa nzito sana kazini. Kila anachokifanya hukumbuka ugomvi wa usiku.

Kama mtu ataondoka nyumbani akiwa hana maelewano na familia yake, ni wazi kwamba siku yake itatawaliwa na giza. Hata kama atajitahidi kuficha, lakini itafikia mahali atashindwa. Kazi inahitaji utulivu.

Ndivyo ilivyo katika maisha, lazima upate mwenzi sahihi ambaye atakupa furaha badala ya mateso. Hapa ndipo tunapojadili jambo moja kubwa na muhimu sana; amani na furaha ya ndoa.

Je, wewe unatarajia nini kwenye ndoa yako ijayo? Unahitaji mafanikio au kuvurunda kila siku kwenye biashara zako? Kama unataka kuwa bora, lazima pia uwe na mwenzi sahihi. Rafiki zangu wengi wanajiandaa kwa mazuri tu kwenye ndoa zao.
Hawana mpango na changamoto na migogoro, hapo watakuwa wanakosea sana.

Kama mnakumbuka vizuri, wiki iliyopita nilieleza kwanza sababu za kujadili mada hii, namna ambavyo baadhi ya watu wanawaza na tatizo lilipo, ambapo imeonekana wengi wanaishi na wapenzi wao kabla ya ndoa, maisha ya kuigiza tu! Yaani anaonesha tabia za ‘kupaka rangi’ lakini akishaingia ndani anabadilika.

Kitu kikubwa ambacho nilikifafanua wiki iliyopita ni tabia ya kuishi maisha yako halisi bila kuigiza. Kufanya hivyo kutampa nafasi mpenzi wako naye aishi maisha yake ya kawaida, mwisho kila mmoja atamjua mwenzake.


KEMEA MAPEMA MATATIZO
Katika kuishi kwako maisha yako halisi, mwenzako naye atakuwa kama wewe. Hiyo ni hatua nzuri maana itakuwa rahisi sana kwako kugundua tabia za mwenzako. Hapo utazijua nzuri na mbaya.

Acha kulea matatizo, bila kujali jinsi, mwambie mpenzi wako tabia ambazo hazikufurahishi. Ili aweze kubadilika kwa urahisi zaidi, unatakiwa kumwambia kwa utaratibu, lakini pia umpe sababu za wewe kukataa tabia zake hizo.

Akiendelea nazo kuwa mkali, wakati mwingine ukali unasaidia. Kwa kukemea, kama ni kweli anakupenda na anahitaji uhusiano wenu uendelee, basi lazima atabadilika. Akifanya hivyo itakuwa vizuri zaidi kwako, maana utakuwa na uhakika angalau kwa asilimia chache kwamba mpenzi wako anakusikiliza.

TABIA ZA ASILI
Rafiki zangu, lazima ufahamu kwamba wakati unapambana na tabia za mpenzi wako zisizokupendeza, zipo tabia nyingine ni za asili. Hazibadiliki. Sasa hapo lazima uwe makini kwa mambo mawili; Mosi, zitakuathiri?

Pili, ni tabia zitakazokugombanisha na jamii? Maana kuna tabia nyingine zinavumilika, lakini je, hazitaleta athari kwa majirani zenu watarajiwa? Haya ni mambo ya kuyatafakari kabla ya kuingia kwenye ndoa.

Mathalani, kuna baadhi ya watu wana viburi au dharau za kuzaliwa! Hata umfanyeje, habadiliki. Unaweza kumwuliza kitu akanyamaza. Ni tabia ya kiburi, lakini kwa sababu amezaliwa akiwa na tabia hiyo, hawezi kuiacha. Sasa hapo lazima ujiulize, utawezana naye?
Utaweza kumvumilia na kiburi chake kwa maisha yenu yote? Huu ni mfano tu rafiki zangu, zipo tabia nyingi za asili, ambazo kwa nafasi yako unaweza kuzichunguza kwa mpenzi wako kabla ya kuchukua uamuzi mzito wa kuingia kwenye ndoa.

KUWA MKWELI
Ukweli ni silaha, ni haki na siku zote humfanya mtu awe huru. Kama kuna jambo ambalo hujalipenda kwa mpenzi wako, haraka mwambie. Acha kukaa na vitu moyoni. Si utaratibu mzuri.

Hata kama nguo zake hazikufurahishi mwambie: “Baby yaani kiukweli ukivaa hizo jeans zako hupendezi kabisa. Nadhani uanze kuvaa suruali za vitambaa.”

Hapo utakuwa umemwambia ukweli wako, kukubaliana na wewe au kukataa kutatokana na mapenzi yenu wewe na yeye. Kama anakupenda atakusikiliza. Kwani anamfurahisha nani huko barabarani zaidi yako? Kuwa mkweli.

UTARATIBU WA KAZI
Suala la kazi kwa baadhi ya wanandoa huwa ni tatizo. Utakuta mwanaume amemkuta binti wa watu anafanya kazi, wamependana na kufunga ndoa. Ghafla anamwambia mwenzake aache kazi!

Ndoa nyingi hasa changa huingia kwenye mgogoro huu. Kwangu mimi, wanandoa wote kufanya kazi ni bora zaidi, maana ile maana ya usaidizi wa mwanamke inakuwa imekamilika. Kwa maisha ya sasa mama kukaa nyumbani siyo ‘dili’ tena.

Hata hivyo, ili kuepusha matatizo, suala hili ni vyema mkajadiliana mapema. Kaa na mwenzako, mwulize: “Lakini dady, vipi kuhusu kazi baada ya kufunga ndoa?”

Anzisha huu mjadala na mwisho muwe na majibu yenye usawa. Mkubaliane kwa pamoja. Vijana wa mtaani wanasema, ‘kwa roho safi’. Hii itakusaidia maana mgogoro huu utakuwa umeisha kabla hata ya ndoa yenu.


VIPI NDUGU ZAKE?

Kama ni kweli una matarajio mazuri kutoka kwa mwenzako, kipengele hiki ni muhimu kabla ya kufanya uamuzi wa kuingia kwenye ndoa.

Lazima uijue vizuri familia yake. Anatoka katika familia ya namna gani? Kabila gani? Ukiachana na hilo, hapa lazima ufahamiane na ndugu zake, japo kidogo na upate muda wa kuwazoea.

Kuna familia nyingine ni wakorofi, kama ukiolewa huko ni tabu tupu. Pengine ukiona katika familia yao, labda wana tabia ya udokozi...si ajabu ukaibiwa hata wewe.
Kweli umempenda na unataka kuishi naye, lakini utaratibu mbaya wa ndugu zake ni kielelezo cha matarajio ya maisha yenu ya ndoa. Kuwa makini.

UNAIJUA AFYA YAKE?

Baadhi ya watu kwa bahati mbaya wana matatizo ya kiafya ya kudumu. Utakuta huyu ana udhaifu wa kusumbuliwa na shinikizo la damu, mwingine vidonda vya tumbo, kifafa n.k.

Ni udhaifu ambao yeyote anaweza kuwa nao. Kwa nini nimegusia hili? Kuna baadhi ya rafiki zangu wanaingia kwenye ndoa wakiwa hawajui matatizo ya wenzao, hivyo kusababisha usumbufu.

Hujui mwenzako anasumbuliwa na nini, mnagombana kidogo unaanza kumpiga, unashangaa ameanguka chini, damu zinaanza kumiminika puani! Si kosa lako, maana hukujua!

Hapa kuna umuhimu mkubwa sana wa kujua afya ya mwenzako. Kama ana maradhi ya kudumu ni vyema ukajua, ili pia ufahamu utakavyotakiwa kuishi naye ndani ya ndoa. Hakikisha unaijua historia ya afya yake vyema. Hakuna maana mbaya kufahamu, isipokuwa utakuwa na uwezo wa kumchukulia kulingana na udhaifu wake.

MILA NA DESTURI

Kuna makabila mengi nchini, kila watu wana mila zao, lazima uzijue japo kwa ufupi. Unaweza kuzungumza naye au ukawashirikisha watu wazima ambao wana ufahamu mkubwa, watakusaidia.

Unaweza kuingia kwenye kabila ambalo mila zake zinaruhusu mwanaume kulala na shemeji yake kama kaka yake hayupo; itakuwaje hapo kama ulikuwa hujui?

Kuna mengi ambayo siwezi kuyaandika yote, lakini jambo kubwa na muhimu kwako hapa ni kuhakikisha unafahamu mila na desturi za mume/ mke wako mtarajiwa.

KUHUSU IMANI ZA DINI

Inapendeza zaidi kama mkioana ndani ya imani moja ya dini. Upo utararibu wa wachumba kufunga ndoa bomani, ambapo kila mmoja huwa na dini yake. Siku za hivi karibuni wengi wanafanya hivyo, lakini si sahihi kwa asilimia mia moja.

Ndoa imara, ukiacha juhudi za wahusika wenyewe hujengwa na hulindwa na imani thabiti ya dini ya wahusika. Mnapokuwa katika imani moja, ni rahisi kumfikia Mungu pamoja katika maombi au kwenda kwa viongozi wa dini pamoja na kupewa ushauri wa kiroho.
Jambo hili lisiwe la mwisho, kama tayari dalili za kuoana zinaonekana wazi, muanze kujadiliana mapema juu ya suala la dini. Lazima muwe dhehebu moja, kama mpo tofuati, mshauriane ili mmoja amfuate mwenzake. Hakuna kinachoshindikana kwenye mazungumzo.

MNIE MAMOJA

Hapa namaanisha kwamba, ili ndoa yenu iwe bora lazima kuanzia mapema muwe na nia moja kwa kila jambo. Sina lugha nyepesi sana ya kudadavua hili, lakini kikubwa ni kwamba mnapaswa kuwa na mawazo ya aina moja kwa maana ya kushirikishana tangu mapema.
Jengeni mazoea ya kushirikishana kila kitu. Hii itawajengea uaminifu na kila mmoja kujiona sehemu ya mwenzake.

Kwa nini yote hayo?
Ndiyo taswira ya kile unachokiendelea ndani ya ndoa. Ikiwa uhusiano wenu awali haukuzingatia niliyoyataja hapo juu, matarajio ya ndoa yako yatakuwa kinyume.

Acha utaratibu wa kuamini kwamba kwenye ndoa kuna furaha, kuna starehe tu, kuna kusaidiana tu. Zipo changamoto ambazo lazima ukubaliane nazo au ujiandae kukutana nazo kuanzia mapema.

Kwa hakika hayo yakifuatwa kwa makini, ndoa yenu itakuwa bora na bila shaka utakuwa na matarajio mema katika ndoa yako ijayo.

Unatarajia nini kutoka kwa mchumba wako

Je, ni kweli kwamba ndoa ni furaha tu? Hakuna huzuni? Hakuna ugomvi? Rafiki zangu, hata viongozi wa dini, wanapofungisha ndoa, husisitiza kuhusu kuvumiliana, kutunzana na kupendana kwa dhati hata katika kipindi cha shida na raha.

Kwa bahati mbaya, baada ya rafiki zetu wanapokea tofauti maneno haya, wanaamini kwa kuambiwa, humaanisha kwamba kupendana labda hata kama fedha ya kula itakosekana nyumbani, mwenzake akiumwa n.k. Huo ni mtazamo tasa. Katika mada hii nitakufumbua, ujue nini zaidi utakutana nacho ukiwa ndani ya ndoa.

KWANINI TUNAJADILI?
Rafiki yangu ipo haja ya kujadiliana juu ya jambo hili tena kirafiki kabisa. Haya ni mambo ambayo sisi vijana tunakutana nayo. Ni wazi kwamba, kila kijana anawaza kuhusu ndoa.

Anawaza kuoa au kuolewa. Anatamani kuwa na familia yake ili aitwe mama au baba, au siyo jamani? Sasa kabla ya kuingia kwenye hizo ndoa ni lazima tuzijue kwanza, hii ndiyo sababu hasa iliyonisukuma kuandika mada hii.

FIKRA ZA WENGI
Kama nilivyoeleza hapo juu, fikra za wengi ni tofauti. Asilimia kubwa wanafikiria zaidi kuhusu maisha mazuri yasiyo na mikwaruzano. Wanawaza kufurahia ndoa na kudhani hakuna changamoto nyingine.
Wapo wanaofikiria hata suala la tendo la ndoa. Kwamba watakuwa huru kukutana kila siku kadiri watakavyoweza kwa kuwa wapo pamoja ndani. Hii ni mitazamo mibaya sana katika ndoa.

Ni kweli unaweza kufanya tendo la ndoa na mwenzako mara nyingi uwezavyo, lakini nani amekudanganya kwamba kila siku utaendelea kumuona kama umuonavyo leo? Amini usiamini, zipo ndoa nyingi zinazolalamikia suala la tendo la ndoa.
Kuna ambao wanadai hawatoshelezwi huku wengine wakilalama kuwa wenzi wao hawataki kabisa kutoa unyumba. Unajua kwa nini? Ama ana mtu mwingine pembeni au amechoshwa na mapenzi ya aina moja kila siku.

(i) Wanaume
Hawa fikra zao huwa kwenye suala la usafi, wanaamini wakiwa kwenye ndoa nyumba itakuwa safi, nguo zitafuliwa, kupikiwa na mambo mengine ya kifamilia.
Akili zao zinakomea hapo tu, hawawazi kuhusu migogoro na namna ya kutatua. Wanaota kuwa na maisha mazuri, kuwa na watoto na kujijengea heshima kwa jamii. Hilo tu, basi!

(ii) Wanawake
Baadhi ya hawa ninaowazungumzia hufikiria kuhusu kuvaa vizuri, kutolewa out, kupata watoto na mengineyo. Kamwe hawana muda wa kufikiria juu ya matatizo ambayo yanaweza kutokea katika maisha ya ndoa.
Hili ni tatizo. Rafiki zangu, maisha ya ndoa hayana furaha siku zote. Kuna wakati dhoruba hutokea na kusababisha mifarakano hivyo kuhitajika umakini wa hali ya juu katika kumaliza tatizo. Si kila siku kuna amani.

TATIZO LIPO WAPI?
Kwa wale ambao wana mitazamo ambayo nimeeleza hapo juu, huwa hawana muda kwanza wa kuwachunguza wapenzi wao, lakini pia wao wenyewe kuonesha tabia zao halisi ili wenzi wao waweze kusoma kama wataweza kuendana nao.
Rafiki zangu, kwa ujumla hatutakiwi kufikiria mazuri pekee kwenye ndoa, kuna mengi ya kuvumiliana. Lakini pia kabla ya kuamua kuingia kwenye ndoa na mwenzako, kipengele kifuatacho hapa chini ni silaha muhimu sana kwako.

ISHI MAISHA YAKO HALISI
Huwezi kumjua mwenzako kama atakuwa anaishi kisanii na wewe. Sikiliza, kwa wiki mnakutana mara mbili tu, tena mnakaa kwa muda usiozidi masaa mawili, si rahisi sana kuweza kujuana tabia zenu halisi.

Pamoja na hayo, wataalamu wa mambo ya mapenzi wanashauri ili mwenzi aweze kuwa wazi zaidi kwa mwenzake ni vyema yeye akaanza kuwa wazi na kuishi maisha yake halisi kwa uwazi. Usijilazimishe kupenda kitu ambacho hukipendi. Kama kuna jambo ambalo analifanya na linakuboa, mwambie ajue ukweli.

Kwanza, uwazi wako kwake utamfanya naye awe wazi kwako. Hatakuwa na sababu ya kuigiza maisha wakati wewe unaishi maisha yako halisi.

Kila mmoja akimjua mwenzake, ndoa haiwezi kuwa na matatizo, maana kila mtu atakuwa anajua anaishi na mtu wa aina gani. Inawezekana kabisa, mmoja wenu akaona tabia za mwenzake zimemshinda. Kama ni kweli na umegundua kwamba kuingia kwenye ndoa ni sawa na utumwa, fanya maamuzi!

NATAMANI sana kuona maisha ya vijana wa sasa yakiwa hayana migogoro, hasa ya mapenzi. Ni furaha yangu kuona vijana wakifanikiwa katika kazi zao na maisha yao kwa ujumla. Rafiki zangu, maisha bora au utaratibu mzuri wa maisha unatokana na uhusiano mwema wa mhusika na mwenzake.

Kama ulikuwa hujui, leo chukua hii elimu, kijana/mtu ambaye amegombana na mpenzi wake usiku uliopita, siku yake huwa nzito sana kazini. Kila anachokifanya hukumbuka ugomvi wa usiku.

Kama mtu ataondoka nyumbani akiwa hana maelewano na familia yake, ni wazi kwamba siku yake itatawaliwa na giza. Hata kama atajitahidi kuficha, lakini itafikia mahali atashindwa. Kazi inahitaji utulivu.

Ndivyo ilivyo katika maisha, lazima upate mwenzi sahihi ambaye atakupa furaha badala ya mateso. Hapa ndipo tunapojadili jambo moja kubwa na muhimu sana; amani na furaha ya ndoa.

Je, wewe unatarajia nini kwenye ndoa yako ijayo? Unahitaji mafanikio au kuvurunda kila siku kwenye biashara zako? Kama unataka kuwa bora, lazima pia uwe na mwenzi sahihi. Rafiki zangu wengi wanajiandaa kwa mazuri tu kwenye ndoa zao.
Hawana mpango na changamoto na migogoro, hapo watakuwa wanakosea sana.

Kama mnakumbuka vizuri, wiki iliyopita nilieleza kwanza sababu za kujadili mada hii, namna ambavyo baadhi ya watu wanawaza na tatizo lilipo, ambapo imeonekana wengi wanaishi na wapenzi wao kabla ya ndoa, maisha ya kuigiza tu! Yaani anaonesha tabia za ‘kupaka rangi’ lakini akishaingia ndani anabadilika.

Kitu kikubwa ambacho nilikifafanua wiki iliyopita ni tabia ya kuishi maisha yako halisi bila kuigiza. Kufanya hivyo kutampa nafasi mpenzi wako naye aishi maisha yake ya kawaida, mwisho kila mmoja atamjua mwenzake.


KEMEA MAPEMA MATATIZO
Katika kuishi kwako maisha yako halisi, mwenzako naye atakuwa kama wewe. Hiyo ni hatua nzuri maana itakuwa rahisi sana kwako kugundua tabia za mwenzako. Hapo utazijua nzuri na mbaya.

Acha kulea matatizo, bila kujali jinsi, mwambie mpenzi wako tabia ambazo hazikufurahishi. Ili aweze kubadilika kwa urahisi zaidi, unatakiwa kumwambia kwa utaratibu, lakini pia umpe sababu za wewe kukataa tabia zake hizo.

Akiendelea nazo kuwa mkali, wakati mwingine ukali unasaidia. Kwa kukemea, kama ni kweli anakupenda na anahitaji uhusiano wenu uendelee, basi lazima atabadilika. Akifanya hivyo itakuwa vizuri zaidi kwako, maana utakuwa na uhakika angalau kwa asilimia chache kwamba mpenzi wako anakusikiliza.

TABIA ZA ASILI
Rafiki zangu, lazima ufahamu kwamba wakati unapambana na tabia za mpenzi wako zisizokupendeza, zipo tabia nyingine ni za asili. Hazibadiliki. Sasa hapo lazima uwe makini kwa mambo mawili; Mosi, zitakuathiri?

Pili, ni tabia zitakazokugombanisha na jamii? Maana kuna tabia nyingine zinavumilika, lakini je, hazitaleta athari kwa majirani zenu watarajiwa? Haya ni mambo ya kuyatafakari kabla ya kuingia kwenye ndoa.

Mathalani, kuna baadhi ya watu wana viburi au dharau za kuzaliwa! Hata umfanyeje, habadiliki. Unaweza kumwuliza kitu akanyamaza. Ni tabia ya kiburi, lakini kwa sababu amezaliwa akiwa na tabia hiyo, hawezi kuiacha. Sasa hapo lazima ujiulize, utawezana naye?
Utaweza kumvumilia na kiburi chake kwa maisha yenu yote? Huu ni mfano tu rafiki zangu, zipo tabia nyingi za asili, ambazo kwa nafasi yako unaweza kuzichunguza kwa mpenzi wako kabla ya kuchukua uamuzi mzito wa kuingia kwenye ndoa.

KUWA MKWELI
Ukweli ni silaha, ni haki na siku zote humfanya mtu awe huru. Kama kuna jambo ambalo hujalipenda kwa mpenzi wako, haraka mwambie. Acha kukaa na vitu moyoni. Si utaratibu mzuri.

Hata kama nguo zake hazikufurahishi mwambie: “Baby yaani kiukweli ukivaa hizo jeans zako hupendezi kabisa. Nadhani uanze kuvaa suruali za vitambaa.”

Hapo utakuwa umemwambia ukweli wako, kukubaliana na wewe au kukataa kutatokana na mapenzi yenu wewe na yeye. Kama anakupenda atakusikiliza. Kwani anamfurahisha nani huko barabarani zaidi yako? Kuwa mkweli.

UTARATIBU WA KAZI
Suala la kazi kwa baadhi ya wanandoa huwa ni tatizo. Utakuta mwanaume amemkuta binti wa watu anafanya kazi, wamependana na kufunga ndoa. Ghafla anamwambia mwenzake aache kazi!

Ndoa nyingi hasa changa huingia kwenye mgogoro huu. Kwangu mimi, wanandoa wote kufanya kazi ni bora zaidi, maana ile maana ya usaidizi wa mwanamke inakuwa imekamilika. Kwa maisha ya sasa mama kukaa nyumbani siyo ‘dili’ tena.

Hata hivyo, ili kuepusha matatizo, suala hili ni vyema mkajadiliana mapema. Kaa na mwenzako, mwulize: “Lakini dady, vipi kuhusu kazi baada ya kufunga ndoa?”

Anzisha huu mjadala na mwisho muwe na majibu yenye usawa. Mkubaliane kwa pamoja. Vijana wa mtaani wanasema, ‘kwa roho safi’. Hii itakusaidia maana mgogoro huu utakuwa umeisha kabla hata ya ndoa yenu.


VIPI NDUGU ZAKE?

Kama ni kweli una matarajio mazuri kutoka kwa mwenzako, kipengele hiki ni muhimu kabla ya kufanya uamuzi wa kuingia kwenye ndoa.

Lazima uijue vizuri familia yake. Anatoka katika familia ya namna gani? Kabila gani? Ukiachana na hilo, hapa lazima ufahamiane na ndugu zake, japo kidogo na upate muda wa kuwazoea.

Kuna familia nyingine ni wakorofi, kama ukiolewa huko ni tabu tupu. Pengine ukiona katika familia yao, labda wana tabia ya udokozi...si ajabu ukaibiwa hata wewe.
Kweli umempenda na unataka kuishi naye, lakini utaratibu mbaya wa ndugu zake ni kielelezo cha matarajio ya maisha yenu ya ndoa. Kuwa makini.

UNAIJUA AFYA YAKE?

Baadhi ya watu kwa bahati mbaya wana matatizo ya kiafya ya kudumu. Utakuta huyu ana udhaifu wa kusumbuliwa na shinikizo la damu, mwingine vidonda vya tumbo, kifafa n.k.

Ni udhaifu ambao yeyote anaweza kuwa nao. Kwa nini nimegusia hili? Kuna baadhi ya rafiki zangu wanaingia kwenye ndoa wakiwa hawajui matatizo ya wenzao, hivyo kusababisha usumbufu.

Hujui mwenzako anasumbuliwa na nini, mnagombana kidogo unaanza kumpiga, unashangaa ameanguka chini, damu zinaanza kumiminika puani! Si kosa lako, maana hukujua!

Hapa kuna umuhimu mkubwa sana wa kujua afya ya mwenzako. Kama ana maradhi ya kudumu ni vyema ukajua, ili pia ufahamu utakavyotakiwa kuishi naye ndani ya ndoa. Hakikisha unaijua historia ya afya yake vyema. Hakuna maana mbaya kufahamu, isipokuwa utakuwa na uwezo wa kumchukulia kulingana na udhaifu wake.

MILA NA DESTURI

Kuna makabila mengi nchini, kila watu wana mila zao, lazima uzijue japo kwa ufupi. Unaweza kuzungumza naye au ukawashirikisha watu wazima ambao wana ufahamu mkubwa, watakusaidia.

Unaweza kuingia kwenye kabila ambalo mila zake zinaruhusu mwanaume kulala na shemeji yake kama kaka yake hayupo; itakuwaje hapo kama ulikuwa hujui?

Kuna mengi ambayo siwezi kuyaandika yote, lakini jambo kubwa na muhimu kwako hapa ni kuhakikisha unafahamu mila na desturi za mume/ mke wako mtarajiwa.

KUHUSU IMANI ZA DINI

Inapendeza zaidi kama mkioana ndani ya imani moja ya dini. Upo utararibu wa wachumba kufunga ndoa bomani, ambapo kila mmoja huwa na dini yake. Siku za hivi karibuni wengi wanafanya hivyo, lakini si sahihi kwa asilimia mia moja.

Ndoa imara, ukiacha juhudi za wahusika wenyewe hujengwa na hulindwa na imani thabiti ya dini ya wahusika. Mnapokuwa katika imani moja, ni rahisi kumfikia Mungu pamoja katika maombi au kwenda kwa viongozi wa dini pamoja na kupewa ushauri wa kiroho.
Jambo hili lisiwe la mwisho, kama tayari dalili za kuoana zinaonekana wazi, muanze kujadiliana mapema juu ya suala la dini. Lazima muwe dhehebu moja, kama mpo tofuati, mshauriane ili mmoja amfuate mwenzake. Hakuna kinachoshindikana kwenye mazungumzo.

MNIE MAMOJA

Hapa namaanisha kwamba, ili ndoa yenu iwe bora lazima kuanzia mapema muwe na nia moja kwa kila jambo. Sina lugha nyepesi sana ya kudadavua hili, lakini kikubwa ni kwamba mnapaswa kuwa na mawazo ya aina moja kwa maana ya kushirikishana tangu mapema.
Jengeni mazoea ya kushirikishana kila kitu. Hii itawajengea uaminifu na kila mmoja kujiona sehemu ya mwenzake.

Kwa nini yote hayo?
Ndiyo taswira ya kile unachokiendelea ndani ya ndoa. Ikiwa uhusiano wenu awali haukuzingatia niliyoyataja hapo juu, matarajio ya ndoa yako yatakuwa kinyume.

Acha utaratibu wa kuamini kwamba kwenye ndoa kuna furaha, kuna starehe tu, kuna kusaidiana tu. Zipo changamoto ambazo lazima ukubaliane nazo au ujiandae kukutana nazo kuanzia mapema.

Kwa hakika hayo yakifuatwa kwa makini, ndoa yenu itakuwa bora na bila shaka utakuwa na matarajio mema katika ndoa yako ijayo.

Unavyopaswa Kufanya unapoachana na mwenzi wako

Kamwe usithubutu kumshusha thamani mwenzi wako wa zamani. Maneno kama ‘alikuwa hanitoshelezi’ na mengine yenye sura ya kumponda hayana nafasi. Maisha yanaendelea, usipoteze muda wako.

Una mengi yanayohitaji utekelezaji wako. Muda wa kumchukia mwenzi wako wa zamani na ule wa kufanya shughuli kwa ajili ya maendeleo yako, utaupanga vipi?
Watu wengi wamekuwa kama mandondocha kwenye mapenzi yao kutokana na tabia ya kushindwa kuchanganua busara za kuachana. Wanakimbilia kuchukia, matokeo yake wanateseka.

Mantiki ya kumchukia mwenzi wako mliyeachana ni matokeo ya kushindwa kuchukulia hali ya kutengana kwenu kama ya kawaida. Unadhani ni tukio kubwa, hivyo unaupa mzigo mzito moyo wako.

CHUKUA MFANO HUU:
Amos anampenda sana Catherine lakini anajua fika kwamba mwenzi wake hajatulia. Hata hivyo anashindwa kujipanga kuchukua hatua muafaka.

Amos anakuwa mtu wa kulipuka, akiudhiwa na mwenzi wake anatangaza kuachana naye bila kutafakari mara mbili. Haishii hapo, anaamka na chuki mtindo mmoja, hata akimkuta barabarani hamsalimii.

Je, hiyo ni dawa? La hasha, kwa kawaida chuki yako itakupeleka katika mawazo mengi. Utamkumbuka kwa mabaya yake lakini hutaishia hapo, utaanza kuyaona mazuri aliyokufanyia.
Ni kipindi hicho ambacho utaanza kuumia zaidi. Utatamani yale mazuri yake. Inawezekana ukakosa aibu na kujikuta wewe mwenyewe ndiyo unaomba msamaha mrudiane.

Ukiwa na chuki na mwenzi wako, maana yake hisia zako bado zipo kwake. Akija kuzungumza na wewe ni rahisi kumsamehe bila kuzingatia uzito wa kitu alichokufanyia.
Nakusisitiza kujua kwamba kinyume cha mapenzi siyo chuki. Ni kutojali (kupotezea). Yaani unapokosana na mwenzi wako, usianze bifu, badala yake anza kumpotezea na usimjali kwa chochote.

Unahitaji kuwa huru na hisia zako. Unapoamua kuacha basi simamia uamuzi wako. Ukizingatia mambo yafuatayo, yatakupa msaada mkubwa wa kuvuka kipindi kigumu cha kuachana na mwenzako.

1. Mara unapoachana na mwenzi wako, jitahidi kadiri uwezavyo kuhakikisha unasitisha mawasiliano naye. Iwe kwa simu, ana kwa ana na mengineyo.

2. Acha kukaribisha hisia kwamba ipo siku wewe na yeye mtarudiana. Amini kuwa hiyo imetoka jumla, kwa hiyo fanya mambo yako, huku ukiamini kwamba mwenzi wa maisha yako anakuja.

3. Fanya mambo chanya kama vile kujifunza vitu vipya, kuongeza ujuzi, kufanya kazi kwa bidii, kujitolea kwa ajili ya watu wengine, kutoa misaada na kufanya mazoezi ya viungo.

Ukiyafanya haya yatakuwezesha kuondoa mawazo hasi kwa mwenzi wako mliyeachana na kuzingatia vitu vya msingi ambavyo vinahusu ujenzi wa maisha yako ya sasa na ya baadaye.

MUHIMU:
Achana na hulka za chuki kwa mwenzi wako wa zamani. Tangu ulipokuwa mdogo mpaka sasa umekutana na marafiki wangapi ambao wengine leo hawamo kwenye kumbukumbu zako?

Unavyopaswa Kufanya unapoachana na mwenzi wako

Kamwe usithubutu kumshusha thamani mwenzi wako wa zamani. Maneno kama ‘alikuwa hanitoshelezi’ na mengine yenye sura ya kumponda hayana nafasi. Maisha yanaendelea, usipoteze muda wako.

Una mengi yanayohitaji utekelezaji wako. Muda wa kumchukia mwenzi wako wa zamani na ule wa kufanya shughuli kwa ajili ya maendeleo yako, utaupanga vipi?
Watu wengi wamekuwa kama mandondocha kwenye mapenzi yao kutokana na tabia ya kushindwa kuchanganua busara za kuachana. Wanakimbilia kuchukia, matokeo yake wanateseka.

Mantiki ya kumchukia mwenzi wako mliyeachana ni matokeo ya kushindwa kuchukulia hali ya kutengana kwenu kama ya kawaida. Unadhani ni tukio kubwa, hivyo unaupa mzigo mzito moyo wako.

CHUKUA MFANO HUU:
Amos anampenda sana Catherine lakini anajua fika kwamba mwenzi wake hajatulia. Hata hivyo anashindwa kujipanga kuchukua hatua muafaka.

Amos anakuwa mtu wa kulipuka, akiudhiwa na mwenzi wake anatangaza kuachana naye bila kutafakari mara mbili. Haishii hapo, anaamka na chuki mtindo mmoja, hata akimkuta barabarani hamsalimii.

Je, hiyo ni dawa? La hasha, kwa kawaida chuki yako itakupeleka katika mawazo mengi. Utamkumbuka kwa mabaya yake lakini hutaishia hapo, utaanza kuyaona mazuri aliyokufanyia.
Ni kipindi hicho ambacho utaanza kuumia zaidi. Utatamani yale mazuri yake. Inawezekana ukakosa aibu na kujikuta wewe mwenyewe ndiyo unaomba msamaha mrudiane.

Ukiwa na chuki na mwenzi wako, maana yake hisia zako bado zipo kwake. Akija kuzungumza na wewe ni rahisi kumsamehe bila kuzingatia uzito wa kitu alichokufanyia.
Nakusisitiza kujua kwamba kinyume cha mapenzi siyo chuki. Ni kutojali (kupotezea). Yaani unapokosana na mwenzi wako, usianze bifu, badala yake anza kumpotezea na usimjali kwa chochote.

Unahitaji kuwa huru na hisia zako. Unapoamua kuacha basi simamia uamuzi wako. Ukizingatia mambo yafuatayo, yatakupa msaada mkubwa wa kuvuka kipindi kigumu cha kuachana na mwenzako.

1. Mara unapoachana na mwenzi wako, jitahidi kadiri uwezavyo kuhakikisha unasitisha mawasiliano naye. Iwe kwa simu, ana kwa ana na mengineyo.

2. Acha kukaribisha hisia kwamba ipo siku wewe na yeye mtarudiana. Amini kuwa hiyo imetoka jumla, kwa hiyo fanya mambo yako, huku ukiamini kwamba mwenzi wa maisha yako anakuja.

3. Fanya mambo chanya kama vile kujifunza vitu vipya, kuongeza ujuzi, kufanya kazi kwa bidii, kujitolea kwa ajili ya watu wengine, kutoa misaada na kufanya mazoezi ya viungo.

Ukiyafanya haya yatakuwezesha kuondoa mawazo hasi kwa mwenzi wako mliyeachana na kuzingatia vitu vya msingi ambavyo vinahusu ujenzi wa maisha yako ya sasa na ya baadaye.

MUHIMU:
Achana na hulka za chuki kwa mwenzi wako wa zamani. Tangu ulipokuwa mdogo mpaka sasa umekutana na marafiki wangapi ambao wengine leo hawamo kwenye kumbukumbu zako?

Unavyopaswa Kufanya unapoachana na mwenzi wako

Kamwe usithubutu kumshusha thamani mwenzi wako wa zamani. Maneno kama ‘alikuwa hanitoshelezi’ na mengine yenye sura ya kumponda hayana nafasi. Maisha yanaendelea, usipoteze muda wako.

Una mengi yanayohitaji utekelezaji wako. Muda wa kumchukia mwenzi wako wa zamani na ule wa kufanya shughuli kwa ajili ya maendeleo yako, utaupanga vipi?
Watu wengi wamekuwa kama mandondocha kwenye mapenzi yao kutokana na tabia ya kushindwa kuchanganua busara za kuachana. Wanakimbilia kuchukia, matokeo yake wanateseka.

Mantiki ya kumchukia mwenzi wako mliyeachana ni matokeo ya kushindwa kuchukulia hali ya kutengana kwenu kama ya kawaida. Unadhani ni tukio kubwa, hivyo unaupa mzigo mzito moyo wako.

CHUKUA MFANO HUU:
Amos anampenda sana Catherine lakini anajua fika kwamba mwenzi wake hajatulia. Hata hivyo anashindwa kujipanga kuchukua hatua muafaka.

Amos anakuwa mtu wa kulipuka, akiudhiwa na mwenzi wake anatangaza kuachana naye bila kutafakari mara mbili. Haishii hapo, anaamka na chuki mtindo mmoja, hata akimkuta barabarani hamsalimii.

Je, hiyo ni dawa? La hasha, kwa kawaida chuki yako itakupeleka katika mawazo mengi. Utamkumbuka kwa mabaya yake lakini hutaishia hapo, utaanza kuyaona mazuri aliyokufanyia.
Ni kipindi hicho ambacho utaanza kuumia zaidi. Utatamani yale mazuri yake. Inawezekana ukakosa aibu na kujikuta wewe mwenyewe ndiyo unaomba msamaha mrudiane.

Ukiwa na chuki na mwenzi wako, maana yake hisia zako bado zipo kwake. Akija kuzungumza na wewe ni rahisi kumsamehe bila kuzingatia uzito wa kitu alichokufanyia.
Nakusisitiza kujua kwamba kinyume cha mapenzi siyo chuki. Ni kutojali (kupotezea). Yaani unapokosana na mwenzi wako, usianze bifu, badala yake anza kumpotezea na usimjali kwa chochote.

Unahitaji kuwa huru na hisia zako. Unapoamua kuacha basi simamia uamuzi wako. Ukizingatia mambo yafuatayo, yatakupa msaada mkubwa wa kuvuka kipindi kigumu cha kuachana na mwenzako.

1. Mara unapoachana na mwenzi wako, jitahidi kadiri uwezavyo kuhakikisha unasitisha mawasiliano naye. Iwe kwa simu, ana kwa ana na mengineyo.

2. Acha kukaribisha hisia kwamba ipo siku wewe na yeye mtarudiana. Amini kuwa hiyo imetoka jumla, kwa hiyo fanya mambo yako, huku ukiamini kwamba mwenzi wa maisha yako anakuja.

3. Fanya mambo chanya kama vile kujifunza vitu vipya, kuongeza ujuzi, kufanya kazi kwa bidii, kujitolea kwa ajili ya watu wengine, kutoa misaada na kufanya mazoezi ya viungo.

Ukiyafanya haya yatakuwezesha kuondoa mawazo hasi kwa mwenzi wako mliyeachana na kuzingatia vitu vya msingi ambavyo vinahusu ujenzi wa maisha yako ya sasa na ya baadaye.

MUHIMU:
Achana na hulka za chuki kwa mwenzi wako wa zamani. Tangu ulipokuwa mdogo mpaka sasa umekutana na marafiki wangapi ambao wengine leo hawamo kwenye kumbukumbu zako?

Heri upweke kuliko mpenzi asiyejua maana III

KATIKA somo lililopita kama nilivyogusia ushauri wa Brandon King na makala yake ya “Be aware with ones heart” nilieleza kuwa ni kosa kubwa kumuona mwenzi wako ana thamani ndogo na wakati huo huo ukawa unatoa kipaumbele kwa watu wa pembeni.

Tafsiri inayotawala katika uhusiano ni kuwa kundi linalosumbua mno na kuonekana ni sugu kwa tabia ya namna hii ni lile ambalo linawahusisha memba wanaoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi pasipo imani kamili.
Wanajaribu na hawana ufahamu kwamba moyo haufanyiwi majaribio.
Hii ndiyo sababu ya kusisitiza kuwa ikiwa hujaamua kupenda basi kaa mbali.

Kuna mengi unayoweza kumsababishia mwenzako, ukampotezea muda huku ukimjengea imani upo naye lakini mwisho anakuja kujikuta anauguza dondo la moyo.
Sikitiko la mahaba linashinda msiba!
Hujaumia subiri usimuliwe.

Moyo unapouma kwa sababu ya mapenzi hakuna kitu cha kupoza. Unaweza kunywa pombe na usilewe, ukabugia dawa za usingizi na usilale.
Kifua kinajaa na kwa sababu inaathiri mfumo wa upumuaji na mapafu nayo huingia katika maumivu.
Sikitiko la mahaba ni hatari, likikufika utapungua uzito kwa kasi bila maelezo ya ziada.

Chakula hakiwezi kupita na macho yanaweza kujaa machozi ilhali unatamani kujizuia. Binadamu tumetofautiana, wapo wanaotamani kupendwa lakini wengine wanawacheza shere wanaowapenda.
Dawa kuu ni kujihadhari na watu wasio na mapenzi ya dhati.

Kuwaepuka kadiri inavyowezekana.

Ni mzuri na anakuvutia lakini heri umuone kwa mbali kwa sababu ukimjaza moyoni atakusumbua.
Atakutoa machozi katika eneo ambalo ulihitaji kufurahi.
Maumivu yako hata yajali kwa sababu hana hisia na wewe.

Atakusaliti bila woga kwa maana hana hofu yoyote juu yako.
Itakuwa ngumu kumuacha, vilevile utaona uamuzi wowote wa kutengana naye ni mateso makubwa kwamba heri uumie ukiwa naye kuliko kuachana.

Usijidanganye ndugu yangu, wewe ni binadamu uliyekamilika, kwa hiyo usitarajie mtu wa pili au wa tatu anaweza kusikia kile kinachokuuma moyoni.

Mateso yaliyopo ndani yako unayajua mwenyewe, kwa hiyo unatakiwa kuwa wa kwanza kujihurumia na kuchukua uamuzi wa kujiokoa na mateso.

Kuna kitu kimoja ambacho unatakiwa kukifahamu; Binadamu ni wa ajabu sana, watayajua yako ya siri na kile ambacho mwenzi wako anakifanya pembeni, lakini hawakwambii badala yake wataketi pembeni kuzungumza. “Aah yule wa ajabu, anadhani kapata mpenzi kumbe kapatikana!”

Wengine utakaa nao meza moja kushauriana mambo mbalimbali, lakini anayekwambia umvumilie mwenzi wako licha ya vitimbi anavyokufanyia, ndiyo huyo huyo akikaa pembeni na watu anawaambia kwa mtindo wa kukucheka kwamba unamng’ang’ania mpenzi bomu.

Lingine ni kuwa unapokuwa na mpenzi ambaye hakuheshimu, thamani yako katika jamii inashuka.
Kukuheshimu si mpaka akutukane, bali vitendo vyake. Kutoka na wapenzi wengine, kujenga mazoea na watu wa jinsia nyingine kiasi kwamba mpaka anahusishwa kwamba ni wapenzi wake.

Mathalan, mpenzi wako anakuwa na urafiki na watu mpaka anafikiriwa anatembea nao.
Hii ni tabia mbaya na haikubaliki, ingawa wapo wazuri wa kutetea. Watasema, sisi ni washkaji ila fahamu mapenzi yenu yanazikutanisha familia mbili. Una ndugu, marafiki, wazazi.

Inakuaje mpenzi wako anahisiwa anatoka na mwanamke mwingine na taarifa zinafika mpaka kwa wazazi wako? Watajua mkwe wao ni kicheche na hilo litakugharimu kwa kiasi kikubwa.

Unatakiwa kulinda thamani, heshima na utu wako, kwa hiyo achana na mtu asiyejua maana!
Unaweza kuona leo inakuuma kwa sababu unaepukana na mtu ambaye unampenda lakini hiyo ni nafuu kwako kesho.
Amini kwamba mwisho wa mateso hayo ya moyo ni furaha kubwa, mwisho utajiuliza:

Ni kipi kilichokuwa kinakufanya uumie kwa muda wote? Upo huru sasa!
Mapenzi maana yake utulivu wa moyo, yaani wewe na mtu wako spesho muogelee katika dimbwi maalum, ninyi wote mkiwa na amani.

Mkishirikiana katika hali zote. Inakuwa hakuna anayewaza la kwake peke yake isipokuwa kwa ajili yenu.
Ukilia anakuwa wa kwanza kukubembeleza, anapogundua amekuudhi ni mwepesi kukuomba msamaha.
Anasoma mabadiliko yako na kukuuliza kile kinachokusumbua.
Anaficha siri zako, anazungumza lugha tamu na hisia zake zote zipo kwako. Kwa wengine haoni hatamani.

USITHUBUTU KULAZIMISHA PENZI

Yamewafika wengi na wameumia, kwa hiyo ni vizuri kuwa makini.
Utauguza donda la moyo lisiloweza kutibika, utakonda wenzako watakucheka, atakugeuza punda afanye anachokitaka.
Ni kazi bure kumpenda mtu asiyekupenda.
Pamoja na maumivu unayoweza kuyapata lakini kuna vitu hivi lazima vikukute kwa huyo mwenzi wako wa kulazimisha.

ATAKUTESA KWA UBINAFSI WAKE

Hana mapenzi ya kweli na wewe, kwa hiyo si kila wakati atakufikiria.
Kama hamjawa kwenye ndoa itakusumbua kwa sababu ni ngumu kufikiria kwa ajili yenu, isipokuwa atawaza kwa matilaba yake. Kama kuoana, utalazimisha wewe lakini yeye hatokuwa na habari.

Mkiwa kwenye ndoa, hatojisikia fahari kutoka na wewe atalazimisha maisha ya kila mmoja kuwa huru kufanya mambo yake.
Nguo atanunua za kwake na hata siku moja hutoona amekununulia. Wewe utafanya mengi kwa ajili yake lakini yeye atabaki na ubinafsi wake.
Atakutesa, pasha moto ubongo!

AKIONA WENGINE ATAHISI NI WAZURI ZAIDI YAKO!

Mtu huishi kwa fikra zake, kwa hiyo kwa sababu hakupendi kwa moyo wake wote inakuwa ngumu kukukubali, hivyo anapokutana na watu wengine barabarani atadhani ni wazuri kuliko wewe. Atababaika hata mbele yako.

Unahitaji heshima ya kiwango bora na kwa kawaida mpenzi wako anapaswa kukuona wewe ni mtu namba moja.
Kama hakupi nafasi hiyo maana yake anapenda nusunusu au hapendi kabisa.
Usikaribishe mateso, fikiria kesho, chukua uamuzi leo.

HASIFU MUONEKANO WAKO, ANA LAKE KICHWANI!
Hujiulizi, kila siku anakuona na hakusifii! Ni wazi kuwa hata kama wewe ni mzuri kiasi gani, unavaa na kupendeza kwa namna bora kabisa lakini mwenzi wako hawezi kukupa pongezi kwa sababu ana lake kichwani.

Ukiona hilo ujue kwamba yupo mtu ambaye anamsifu kwa sababu ndiye anayemkubali, na wewe utasifiwa na wengine.
Inauma mwenzi wako kukuacha nyumbani na kwenda kumwaga sifa pembeni, wakati na wewe unazihitaji.
Una thamani kubwa, pigania utulivu wa moyo wako!

Heri upweke kuliko mpenzi asiyejua maana III

KATIKA somo lililopita kama nilivyogusia ushauri wa Brandon King na makala yake ya “Be aware with ones heart” nilieleza kuwa ni kosa kubwa kumuona mwenzi wako ana thamani ndogo na wakati huo huo ukawa unatoa kipaumbele kwa watu wa pembeni.

Tafsiri inayotawala katika uhusiano ni kuwa kundi linalosumbua mno na kuonekana ni sugu kwa tabia ya namna hii ni lile ambalo linawahusisha memba wanaoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi pasipo imani kamili.
Wanajaribu na hawana ufahamu kwamba moyo haufanyiwi majaribio.
Hii ndiyo sababu ya kusisitiza kuwa ikiwa hujaamua kupenda basi kaa mbali.

Kuna mengi unayoweza kumsababishia mwenzako, ukampotezea muda huku ukimjengea imani upo naye lakini mwisho anakuja kujikuta anauguza dondo la moyo.
Sikitiko la mahaba linashinda msiba!
Hujaumia subiri usimuliwe.

Moyo unapouma kwa sababu ya mapenzi hakuna kitu cha kupoza. Unaweza kunywa pombe na usilewe, ukabugia dawa za usingizi na usilale.
Kifua kinajaa na kwa sababu inaathiri mfumo wa upumuaji na mapafu nayo huingia katika maumivu.
Sikitiko la mahaba ni hatari, likikufika utapungua uzito kwa kasi bila maelezo ya ziada.

Chakula hakiwezi kupita na macho yanaweza kujaa machozi ilhali unatamani kujizuia. Binadamu tumetofautiana, wapo wanaotamani kupendwa lakini wengine wanawacheza shere wanaowapenda.
Dawa kuu ni kujihadhari na watu wasio na mapenzi ya dhati.

Kuwaepuka kadiri inavyowezekana.

Ni mzuri na anakuvutia lakini heri umuone kwa mbali kwa sababu ukimjaza moyoni atakusumbua.
Atakutoa machozi katika eneo ambalo ulihitaji kufurahi.
Maumivu yako hata yajali kwa sababu hana hisia na wewe.

Atakusaliti bila woga kwa maana hana hofu yoyote juu yako.
Itakuwa ngumu kumuacha, vilevile utaona uamuzi wowote wa kutengana naye ni mateso makubwa kwamba heri uumie ukiwa naye kuliko kuachana.

Usijidanganye ndugu yangu, wewe ni binadamu uliyekamilika, kwa hiyo usitarajie mtu wa pili au wa tatu anaweza kusikia kile kinachokuuma moyoni.

Mateso yaliyopo ndani yako unayajua mwenyewe, kwa hiyo unatakiwa kuwa wa kwanza kujihurumia na kuchukua uamuzi wa kujiokoa na mateso.

Kuna kitu kimoja ambacho unatakiwa kukifahamu; Binadamu ni wa ajabu sana, watayajua yako ya siri na kile ambacho mwenzi wako anakifanya pembeni, lakini hawakwambii badala yake wataketi pembeni kuzungumza. “Aah yule wa ajabu, anadhani kapata mpenzi kumbe kapatikana!”

Wengine utakaa nao meza moja kushauriana mambo mbalimbali, lakini anayekwambia umvumilie mwenzi wako licha ya vitimbi anavyokufanyia, ndiyo huyo huyo akikaa pembeni na watu anawaambia kwa mtindo wa kukucheka kwamba unamng’ang’ania mpenzi bomu.

Lingine ni kuwa unapokuwa na mpenzi ambaye hakuheshimu, thamani yako katika jamii inashuka.
Kukuheshimu si mpaka akutukane, bali vitendo vyake. Kutoka na wapenzi wengine, kujenga mazoea na watu wa jinsia nyingine kiasi kwamba mpaka anahusishwa kwamba ni wapenzi wake.

Mathalan, mpenzi wako anakuwa na urafiki na watu mpaka anafikiriwa anatembea nao.
Hii ni tabia mbaya na haikubaliki, ingawa wapo wazuri wa kutetea. Watasema, sisi ni washkaji ila fahamu mapenzi yenu yanazikutanisha familia mbili. Una ndugu, marafiki, wazazi.

Inakuaje mpenzi wako anahisiwa anatoka na mwanamke mwingine na taarifa zinafika mpaka kwa wazazi wako? Watajua mkwe wao ni kicheche na hilo litakugharimu kwa kiasi kikubwa.

Unatakiwa kulinda thamani, heshima na utu wako, kwa hiyo achana na mtu asiyejua maana!
Unaweza kuona leo inakuuma kwa sababu unaepukana na mtu ambaye unampenda lakini hiyo ni nafuu kwako kesho.
Amini kwamba mwisho wa mateso hayo ya moyo ni furaha kubwa, mwisho utajiuliza:

Ni kipi kilichokuwa kinakufanya uumie kwa muda wote? Upo huru sasa!
Mapenzi maana yake utulivu wa moyo, yaani wewe na mtu wako spesho muogelee katika dimbwi maalum, ninyi wote mkiwa na amani.

Mkishirikiana katika hali zote. Inakuwa hakuna anayewaza la kwake peke yake isipokuwa kwa ajili yenu.
Ukilia anakuwa wa kwanza kukubembeleza, anapogundua amekuudhi ni mwepesi kukuomba msamaha.
Anasoma mabadiliko yako na kukuuliza kile kinachokusumbua.
Anaficha siri zako, anazungumza lugha tamu na hisia zake zote zipo kwako. Kwa wengine haoni hatamani.

USITHUBUTU KULAZIMISHA PENZI

Yamewafika wengi na wameumia, kwa hiyo ni vizuri kuwa makini.
Utauguza donda la moyo lisiloweza kutibika, utakonda wenzako watakucheka, atakugeuza punda afanye anachokitaka.
Ni kazi bure kumpenda mtu asiyekupenda.
Pamoja na maumivu unayoweza kuyapata lakini kuna vitu hivi lazima vikukute kwa huyo mwenzi wako wa kulazimisha.

ATAKUTESA KWA UBINAFSI WAKE

Hana mapenzi ya kweli na wewe, kwa hiyo si kila wakati atakufikiria.
Kama hamjawa kwenye ndoa itakusumbua kwa sababu ni ngumu kufikiria kwa ajili yenu, isipokuwa atawaza kwa matilaba yake. Kama kuoana, utalazimisha wewe lakini yeye hatokuwa na habari.

Mkiwa kwenye ndoa, hatojisikia fahari kutoka na wewe atalazimisha maisha ya kila mmoja kuwa huru kufanya mambo yake.
Nguo atanunua za kwake na hata siku moja hutoona amekununulia. Wewe utafanya mengi kwa ajili yake lakini yeye atabaki na ubinafsi wake.
Atakutesa, pasha moto ubongo!

AKIONA WENGINE ATAHISI NI WAZURI ZAIDI YAKO!

Mtu huishi kwa fikra zake, kwa hiyo kwa sababu hakupendi kwa moyo wake wote inakuwa ngumu kukukubali, hivyo anapokutana na watu wengine barabarani atadhani ni wazuri kuliko wewe. Atababaika hata mbele yako.

Unahitaji heshima ya kiwango bora na kwa kawaida mpenzi wako anapaswa kukuona wewe ni mtu namba moja.
Kama hakupi nafasi hiyo maana yake anapenda nusunusu au hapendi kabisa.
Usikaribishe mateso, fikiria kesho, chukua uamuzi leo.

HASIFU MUONEKANO WAKO, ANA LAKE KICHWANI!
Hujiulizi, kila siku anakuona na hakusifii! Ni wazi kuwa hata kama wewe ni mzuri kiasi gani, unavaa na kupendeza kwa namna bora kabisa lakini mwenzi wako hawezi kukupa pongezi kwa sababu ana lake kichwani.

Ukiona hilo ujue kwamba yupo mtu ambaye anamsifu kwa sababu ndiye anayemkubali, na wewe utasifiwa na wengine.
Inauma mwenzi wako kukuacha nyumbani na kwenda kumwaga sifa pembeni, wakati na wewe unazihitaji.
Una thamani kubwa, pigania utulivu wa moyo wako!