Friday, March 27, 2009

Maambukizo ya HPV

Maambukizo ya HPV

Human Papilloma Virus (HPV) ni maambukizo yanayotokea sana wanawake na huambukizwa kwa kufanya ngono, unapata maambukizo haya hata ukitumia kinga (Condom). Baadhi ya maambukizo haya huweza kusababisha Saratani iitwayo "Cervical" au Saratani ya Kizazi ambayo inaweza kusababisha usiweze kushika mimba/zaa ktk maisha yako yote au maambukizo mengine huko ukeni ambayo sio yale ya Ngono tunayoyajua nakutajia kila siku.

Hakuna dalili zozote za Saratani hii ya kizazi lakini ukiwahi kujua kuwa unayo kwa kufanya kipimo kiitwacho "Smear" basi unakuwa umeokoa maisha yako kwani Saratani hii inaua wanawake sambamba na ile ya Matiti.

Mwanamke anaeanza ngono mapema (chini ya miaka 21) anakuwa kwenye hatari kubwa ya kupata Saratani hii na wale wanaoanza Ngono ndani ya miaka 20 huwa x2 kwenye hatari ya kupata Saratani hii.

Tumia Condom

Mpenzi wangu hataki kuvaa kondomu

Kutumia kondom ya wanawake

Kutumia kondom ya wanaume

HIV na Ukimwi barani Afrika

Ngono Salama


Mapenzi salama

Nilikatwa Kisimi

Nilikatwa Kisimi


"Nina tatizo ambalo naona waweza kunisaidia mawazo, mimi ni mwanamke ambaye nimekeketwa nilipokuwa mdogo, kutokana na mila za kwetu kipindi kile. Katika kufanya mapenzi na mpenzi wangu huwa nacum na siku zingine huwa sifiki, siku akiniandaa vizuri huwa naenjoy na huwa nacum hata mara 2 kwenye mzunguko mmoja. Tatizo langu ni kwamba naamini kuwa wenye vinembe huwa wanafaidi mapenzi zaidi na zaidi kuliko tuliokeketwa, je kuna njia yeyote ya kitaalamu ama dawa yeyote inayoweza kurudisha kinembe kilichokatwa?"

JIBU-Kwanza kabisa napenda kukupongeza kwa kuwa wazi ktk kulielezea swala lako. Ni jambo la kumhsukuru Mungu kuwa pamoja na kukeketwa bado una uwezo au niseme umejaaliwa kupata utamu wa kufanya ngono/mapenzi kwenye kona nyingine za uke wako hasa ndani ambwako wanawake wengi hawajui utamu wake.

Napenda nikuhakikishie tu kuwa utamu wa kwenye kisimi
(kinembe) haufikii kabisa ule wa ndani ya uke hasa kama umejaaliwa kusikilizia/kupata utamu huo kisimini na ndani ya uke. Kwa mwanamke ambae hajawahi kabisa kupata utamu wa kungonoana (juu kwa juu au ule wa ndani) kwa sababu tofauti kuanzia mpenzi hataki au hajui kucheza namwili wako mpaka matatizo mengine ya kiafya basi Kisimi ni njia pekee na rahisi ya kumfanya apate uzoefu au idea ya utamu wa ngono ulivyo.

Kwa wewe kufanikiwa kufika kileleni ukiwa huna kisimi nadhani unafaidi zaidi kuliko yule ambae ana kisimi lakini hafiki kileleni uume ukiwa ndani ya uke.

Nasikitika kusema kuwa hakuna dawa ya kurudisha kisimi/kinembe kwani kisimi sio kiungo kinachokua siku hadi siku na vilevile pale mahali hapo palipokuwa na kisimi palikuwa jeraha ambalo limepona na kuwa ni kovu na juu ya kovu huwa hapajitokezi/kua kitu hata kipele huwa hakioti juu ya kovu.

Kuna njia ya kitaalamu (Plastic Surgery) ambapo huumba/tengeneza kisimi cha bandia (kutokana na sehemu ya nyama mwili mwako) kisha wanaunganisha na mabaki ya "nerves" za kisimi (kwenye jeraha) lakini inategemea zaidi na walivyokiondoa, inasemekana baadhi huwa hawaondolewi sana na wengine wanakwanguliwa kabisa. Upasuaji huu unagharimu pesa nyingi.


Ulimi Kisimini-Siri Ya Mwanamke Kufika Kileleni

Jinsi ya Kufurahisha mwanamke Katika Ngono

Ukamilifu wa mwanamke katika Ngono

Sehemu tofauti za utamu wa ngono kwa wanawake

Jinsi ya Kufurahisha mwanamke Katika Ngono