Saturday, December 24, 2011

Utafiti Unaonyesha Kwamba Wanawake Hubakwa na Waume Zao

ubakaji nyumbani

Tafiti zilizofanywa na wataalama wa masuala ya afya na jamii zinadai kuwa baadhi ya wanawake waliomo katika ndoa hukumbana na kadhia ya kubakwa na wanaume zao na pia hudhalilishwa. Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali ambalo hujishughulisha na Afya na Maendeleo ya Mtoto-(KIWOHEDE), Justa Mwaituka amesema kuwa wanawake wengi walio kwenye ndoa wananyanyaswa na waume zao kwakuwa wanalazimishwa kufanya mapenzi kinyume na maumbile pamoja na kufanya kwa njia ya mdomo.

"Iringa tumekutana na wanawake ambao wamezikimbia ndoa zao kutokana na kuingiliwa kinyume na waume zao pamoja na kulazimishwa kufanya ngono kwa njia ya MDOMO"anasema Mwaituka.


Source Mwananchi.

Ngono Kabla ya Kuoana: Biblia Inasema Nini

Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?


Swali: "Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?"

Jibu: Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi yanayokubalika mbele za Mungu (waebrania 13:4).

Kushirikiana katika ngono kabla ndoa kumeenea sana kwa sababu nyingi. Mapenzi yanastarehesha. Mungu aliyaumba hivyo. Anawataka wanaume na wanawake wafurahie kitendo cha ngono (ndani ya ndoa). Hata hivyo, lengo la msingi la ngono si starehe bali kuzaana tukaongezeke. Hivyo tunazuiwa kufanya kitendo cha ngono kabla ndoa ili tusijipatie watoto tusiowatarajia. Kama jambo hili lingezingatiwa, magonjwa ya zinaa na wamama wasioolewa na kuavya mimba na kadhalika kungepungua. Kujizuia kunaokoa maisha, kunalinda watoto wachanga na kuleta ladha halisi ya ngono pamoja na heshima kwa Mungu.

FROM